NA MUSSA KHALID,DAR ES
SALAAM
Baraza la Madiwani wa
Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam limeitaka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia muongozo na kuangalia
namna ya kutowalipisha madiwani ushuru wa maegesho kwani wao ndio wanaidhinisha
fedha za wao kutengeneza barabara.
Hayo yamejiri leo
jijini Dar es salaam katika kikao cha Baraza la Madiwani wa jiji hilo ambacho
kimeongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji na Mwenyekiti wa baraza hilo Omary
Kumbilamoto wakati wakijadili taarifa za utekelezaji kamati mbalimbali kuanzia
kipindi cha Julai mpaka Septemba mwaka huu sambamba na kumuapisha Diwani mpya
wa kata ya Buyuni.
Madiwani hao wamesema
wanakumbana na changamoto pindi wanapoegesha vyombo vya vyao vya usafiri kwa
kulipishwa ushuru hivyo wameeleza kuwa ni vyema TARURA ikawafutia tozo hizo
kutokana na kuwa wao wanawahudumia wananchi.
Akijibu maazimio ya
wajumbe hao wa baraza la madiwani kuhusu msamaha wa ushuru wa maegesho,Meneja
wa TARURA Ilala Samweli Ndoveni amesema atahakikisha analishughulikia suala hilo
ili liweze kupatikana ufumbuzi.
Kuhusu suala la ujenzi
wa barabara Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Kumbilamoto amesema
wamekubaliana na TARURA ndani ya mwezi mmoja madiwani wafanye mapitio ya
taarifa ya maeneo yao ili kuanza uboreshaji barabara hizo.
Katika Hatua nyingine imeelezwa kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam imekusanya takriban Tsh.Bill 17.7 sawa na asilimia 95 katika kipindi cha robo ya kwanza kuanzia mwezi Julai mpaka septemba mwaka huu kutoka katika vyanzo vya ndani na ruzuku serikalini.
Post a Comment