NHIF YAWATAKA WANANCHI KUJIUNGA NA MFUKO WA BIMA YA AFYA


Afisa Masoko wa Huduma kwa wanachama kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Luhende Andrew Singu (picha na Mussa Khalid)

................................

NA MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM

Watanzania wametakiwa kupenda kujiunga na mifuko ya Bima ya Afya ili kuwa salama kwa matibabu kutokana na na kuwa ugonjwa hauipi hodi.

Akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi leo jijini Dar es salaam katika muendelezo wa maonyesho ya wiki ya kifedha Afisa Masoko wa Huduma kwa wanachama kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Luhende Andrew Singu ambapo amesema ni vyema wananchi wakaacha utamadui wa zamani kwa kuwapigia ndugu na jamaa pindi wanapougua hivyo ni vyema wakajiunga na mfuko huo ilikupata msaada.

Singu amewataka watanzania kutambua kuwa Afya ndio kila kitu na hawatoweza kuwa na afya bora kama hawana njia bora ya kupata matibabu hivyo wanapokuwa na bima ya afya itawasaidia pindi wanapokuwa na changamoto za kiafya.

‘Tupo hapa kwenye maadhimisho ya wiki ya fedha kwa shughuli kubwa moja kuhudumia wananchi na kimsingi kuwapa elimu kuhusiana na afya na elimu yetu hii inahusiana na fedha kwa sababu kama mtu huna afya nzuri utajikuta unatumia fedha nyingi lakini ungekuwa umejiunga na mfuko huo ungepata msaada’amesema Singu

Aidha Singu amesema kumekuwa na muako mkubwa kwa wananchi kujiunga na mfuko huo kwani takwimu zinaonyesha kuna zaidi ya watanzania Mill. 4 wanaohudumia na Bima ya Afya huku malengo lao yakiwa ni kufika asilimia zaidi ya 50.

Hata hivyo Singu amesema kuwa mfuko huo umekuwa na mchango mkubwa katika uboreshaji wa huduma ambao umepelekea kupatikana na kwa huduma ambazo awali hazikutolewa ndani ya nchi.

0/Post a Comment/Comments