RC MAKALLA NA BODABODA MAMBO SAFI.


Wakubaliana na Kuunda Kamati ya utaratibu wa vituo na uingiaji na utokaji Mjini*.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Amos Makalla* ametoa muda wa *Miezi mitatu* kwa Shirikisho la *Vyama vya waendesha Bodaboda* Jijini humo kuweka *Mpango kazi* kuwapanga vizuri Bodaboda ikiwa ni pamoja na utaratibu rasmi wa *kuingia mjini na kutoka*  ili kuondoa hali *uholela wa kuingia mjini unayoendelea kwa Sasa.*

RC Makalla* ametoa maazimio hayo wakati wa kikao Cha pamoja baina ya *Viongozi wa Bodaboda, Jeshi la Polisi, LATRA, TARURA na TANROAD* kilicholenga kujadili *zuio la Bodaboda kuingia mjini* lililokuwa limetolewa na Jeshi la Polisi.

Miongoni mwa *maazimio yaliyotolewa na kikao hicho* na yanapaswa kufanyiwa kazi na *Kamati*  iliyoundwa ni pamoja na shughuli za Bodaboda kufanyika sambamba na *kulinda taswira ya Jiji, Uwepo wa vituo rasmi vya Bodaboda vinavyotambulika, Uvaaji wa Sare, Kofia ngumu pamoja na Bodaboda kuwa sehemu ya kuwafichua wahalifu.*

Aidha *RC Makalla* amesema baada ya kupatiwa *Mapendekezo ya Kamati* atahitisha kikao cha *Kamati ya Ulinzi na Usalama* ili kuweka mazingira wezeshi ya kuhakikisha *suala la kuingia mjini linafanyika kwa kuzingatia taratibu.*

Hata hivyo *RC Makalla* amesema Serikali ya awamu ya sita Chini ya *Rais Samia Suluhu Hassan* inathamini *kazi ya Bodaboda* Kutokana na shughuli hiyo *kutoa ajira kwa idadi kubwa ya Vijana.*

Nao baadhi ya *Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya waendesha Bodaboda* akiwemo *Said Kagomba* ambae ndio Mwenyekiti wa Shirikisho ameishukuru Serikali kwa *kukaa meza moja* na Shirikisho Kuangalia namna Bora ya kushughulikia Jambo hilo na wameahidi kushirikiana na Serikali kuweka mazingira Bora ya biashara hiyo ili Bodaboda wa Dar es salaam wawe mfano mzuri wa kuigwa.


0/Post a Comment/Comments