SABABU NZITO ZA WAUMINI KUHAMA MAKANISA YAWEKWA HADHARANI.

Askofu  mkuu   wa  Kanisa  la  Anglikana  la  Kiinjili  Tanzania  Askofu   Ainea   Kunenha akimsimika Nae  mchungaji  Fredi  Mtevi kuwa Mchungaji wa Kanisa la Anglikana la Kiinjili.

.....................................

NA SALYIM BITCHUKA

Viongozi  wa   Makanisa   hapa  nchini wameaswa   kuwa  na   umoja , Upendo  na  Ushirikiano  kwa  kuwa  ndio  njia  pekee  itakayowezesha   wachungaji , Maaskofu  na  waumini  wao  kuitangaza  injili  ya  kweli.

Kauli  hiyo  imetolewa  mwishoni  mwa  wiki  katika  Kanisa  la  Anglikana  la Kiinjili  Tanzania  Parishi  ya  Keko  Mwanga   jijini  Dar  es  Salaam wakati  wa  Ibada  ya  Jumapili  iliyoendana   na  tukio  la Kusimikwa  kwa   Mchungaji   Fredi  Mtevi .

Akizungumza   mara  baada  ya  Ibada  hiyo  Askofu  mkuu   wa  Kanisa  la  Anglikana  la  Kiinjili  Tanzania  Askofu   Ainea   Kunenha  amesema  kuna  haja  ya  Viongozi   wa  Makanisa  kutoa  elimu  iliyo  sahihi  ili  Kanisa  liweze  kusonga  mbele  huku  akisisitiza  umoja  na  ushirikiano  katika  hilo.

Kwa  upande  wao  baadhi  ya  Maskofu  waliohudhuria  Ibada  hiyo  akiwemo  Askofu  Frederick  Chigwaba  Kutoka  Dayosisi  ya  Morogoro  na  Mchungaji   Isaya  Lazaro  Chiyungu  kutoka   kanisa  la Anglikana  la Kiinjili  Tanzania  Parishi  ya  Keko  Mwanga (Mlima  wa  Makimbilio )  jijini  Dar  es  Salaam kwa  pamoja  wamesema  umoja  na  mshikamano   walionaona ndio  siri  kubwa  ya  kufanikiwa  kwa  kanisa  hilo  huku  wakisisitiza   waumini  wao   kupenda  elimu.

Nae  mchungaji  Fredi  Mtevi  akizungumza   mara  baada  ya  kusimikwa  Uchungaji   amesema  lengo la kuhamia  kanisa  hilo na kusimikwa  ni  kwenda  kutoa  huduma  kwa  kuwa  Mungu  hana  mipaka huku  akisisitiza  kuwa  msingi  mkubwa  wa  Kanisa  ni  Elimu.

‘Waumini wengi wamekuwa wakihama kutoka kanisa moja kwenda kanisa linguine kutokana na kumtafuta Mungu wa kweli’amesema Mchungaji Fredi

Kanisa  la  Anglikana  la  Kiinjili  Tanzania   limepunguza   madaraka  ya  Maaskofu huku  likijikita  zaidi  katika  kutoa  huduma  kwa jamii   lakini  bado kwa sehemu  kubwa   linafuata  maadili  ya  Kanisa  la  Anglikana .

0/Post a Comment/Comments