SERIKALI YAOMBWA KUFUNDISHA WATAALAMU WATAKAO SAIDIA KILIMO CHA MWANI.



Mkulima wa Mwani kutoka kikundi cha Msichoke Mlingotini Bagamoyo Mkoa wa Pwani Machano Ally Jingalao

..................................... 

NA MUSSA KHALID.

Serikali imeshauriwa kuonyesha muamko katika zao la Mwani kwa kuwafundisha wataalamu wengi watakaosaidia kukiendeleza kilimo hicho ili kukuza uchumi wan chi kupitia viwanda.

Akifanya mahojiano maalum na mwandishi wa habari hizi leo jijini Dar es salaam Mkulima wa Mwani kutoka kikundi cha Msichoke Mlingotini Bagamoyo Mkoa wa Pwani Machano Ally Jingalao amesema kutokana na watu kukosa uelewa wa zao hilo linaloota baharini imesababisha kuwepo kwa changamoto ya wateja

Mzee Jingalao amesema awali walipokuwa wakilima zao hilo walikuwa wakiwauzia matajiri kutokana na wao kuwa na mfumo mzuri na  utaratibu walikokuwa wakitumia katika manunuzi.

‘Tulipoanza kuvuna Mwani mwaka 1995 tulikuwa tunawauzia matajiri walikuwa wanakuja kuchukua Mwani huu kwa bahati mbaya au nzuri wenzetu walikuwa na utaratibu mzuri sababu walikuwa wanakusaidia kamba mpaka boto lakini wakati wakupanga bei hawatushirikishi hivyo tukaamua kuachana nao’amesema Mzee Jingalo

Aidha Mzee Jingalao amesema ni vyema kwa wataalamu ambao wamekwenda kusoma masuala ya Mwani wakirudi wajihusishe na masuala ya bahari kwani imesheheni mazao mengi ambayo yanaweza kusaidia kukuza uchumi wan chi.

Katika Hatua nyingine Mzee Jingalao amesema changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa inaweza kusababisha Zao hilo la Mwani kubadilika rangi na kuwa la kijana.

Hata hivyo faida ya Zao la Mwani limekuwa likitumika kwa kutengeneza Sabuni, Mafuta ya kujipaka, shampuu na vyakula vya kama Juisi,keki, jam, kachumbari na kupikwa kama mboga sambamba na utengenezaji wa dawa za Binaaadamu, vipodozi na chakula cha mifugo.

0/Post a Comment/Comments