Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI David Silinde ameuagiza uongozi wa wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa kuongeza nguvu ya usimamizi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika halmshauri ya Sumbawanga baada kukagua na kukuta hali si nzuri wakiwa bado wapo nyuma sana katika ujenzi.
Hayo ameyasema akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari ya Mpui na kukuta bado wapo katika hatua ya ujenzi wa msingi katika madarasa nane ambayo wamepewa kiasi cha shilingi milioni 160 na zikiwa zimebaki siku 19 kukabidhi miradi hiyo ofisi ya Rais TAMISEMI ili kuruhusu wanafunzi wa kidato cha kwanza waliyopangiwa kuanza kuyatumia ikiwa ni tofauti na halmashauri ambazo amezipitia katika mkoa wa Songwe ikiwemo mji wa Tunduma ambao wanamalizia kupaka rangi wakabidhi mwisho wa mwezi huu.
Aidha Naibu Waziri Silinde amemtaka Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryoba na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauli ya wilaya ya Lightness Msemo Sumbawanga kuhakikisha ujenzi huo wa madarasa katika shule zote zenye ujenzi kuanza kufanya kazi usiku na mchana ili kukimbizana na tarehe ya kukabidhi miradi hiyo na kuunda timu ya wataalam kuanza kufatilia miradi yote kwa mda wote ili kurahisisha kasi ya ujenzi.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Silinde amewataka baadhi ya madiwani ambao wanakwamisha miradi ya serikali ikiwemo ujenzi wa madarasa nchini na kua hatakua tayari kuwafimbia macho wote watakao husika kukwamisha shughuli za maendeleo na hatua za kinidhamu zitachukuliwa juu yao.
Akitoa taarifa kwa Naibu Waziri Silinde mkuu wa shule ya sekondari Mpui Eddah Mbuba amesema sababu kubwa ya kuchelewa kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa hayo ni kutokana na upungufu wa maji shuleni hapo ambapo yanakatika mala kwa mala hivyo kufanya ujenzi kusuasua kuendelea lakini wanauhakika mpaka ifikapo tarehe ya kukabidhi watakua washamaliza.
Aidha Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryoba amemuahaidi Naibu Waziri Silinde kua watajenga usiku na mchana katika ubora na thamani ya majengo na washafunga taa katika shule zote ambazo bado zipo nyuma na wamepokea maelekezo yote watahakikisha mpaka siku ya kukabidhi madarasa yote yatakua tayari.
Post a Comment