THRDC,LHRC NA SAVE THE CHILDREN WATOA TAHMINI YA MAPENDEKEZO YA UPR 2021

Mratibu kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania THRDC, Bw. Onesmo Olengurumwa

..........................
NA SALIM BITCHUKA

Serikali  ya  Jamhuri  ya  Muungano  imetakiwa  kufikiria  na  kuyakubali  mapendekezo  ambayo  hayajakubaliwa  katika  tathmini  ya  mapitio  ya  hali ya Haki  za  Binadnu  (UPR)  kupitia   mkutano 39.

Hayo  yameelezwa  jana jijini Dar es Salasm  na  Mtandao wa wawateyezi wa haki za binadamu ( THRDC) wakishirikiana  na Kituo cha Sheria na haki  za  Binadamu  ( LHRC)  Pamoja   na Save  the Children   wakati  wa  wakitoa  tathmini  ya  Ripoti  ya  Kikao cha  tatu cha  Mapitio  ya  Hali  ya Haki  za  Binadamu  ( UPR) 2021.

Akiwasilisha  ripoti hiyo  Mratibu kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania THRDC, Bw. Onesmo Olengurumwa, amesema  Serikali   inapaswa  kuwashirikisha  wadau  wengine  wa  haki  za  Binadamu  hususan Asasi  za Kiraia  na  Nchi  wanachama  zilizotoa  mapendekezo  ili  kujadili  uwezekano  wa kuyaboresha   kulingana  na mazingira  halisi  ya  nchi.

Kwa  upande  wake  Mkurugenzi  Utetezi  na Maboresho  LHRC  Fulgence  Masawe  na  Mtaalamu  wa  Utekelezaji  wa  Haki  za   Watoto kutoka   Save The Children   Wilbert  Muchuguzi  wamesema  serikali  inapaswa  kuangalia  mapendekezo  yaliyotolewa  upya  hasa  yale  yanayogusa  haki  za  msingi  ikiwemo  haki  za  kiraia  na Kisiasa.

Jamhuri  ya  Muungano  wa Tanzania kama  nchi  Mwanachama wa  Umoja  wa Mataifa imekuwa  ikishiriki  katika  mchakato   wa Mapitio  ya Hali  ya  Haki  za  Binadamu   na mwaka  huu  2021 Tanzania imefanya  Mapitio  ya  Tatu  ya UPR katika  mkutano  wa  39   ambapo  mapendekezo  252 yalitolewa  kutoka  nchi  mbalimbli

0/Post a Comment/Comments