TIO YASULUHISHA MIGOGORO YA BIMA ZAID YA 1000.


Msajili wa Malalamiko kutoka Ofisi Msuluhishi wa Migogoro ya Bima Magreti Mngumi wakati akifanya mwandishi wa habari hizi katika maonesho ya huduma za kifedha yanayoendelea katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam (picha na Mussa Khalid)

....................................

NA MUSSA KHALID

 Imeelezwa kuwa takriban migogoro zaidi ya 1000 imesuluhishwa na Ofisi ya msuluhishi wa migogoro ya Bima nchini huku kila mwaka ikisuluhishwa migogoro zaidi ya 100 hadi 200 katika fidia na kukataliwa kwa madai ya Bima.

Kauli hiyo imetolewa na Msajili wa Malalamiko kutoka Ofisi Msuluhishi wa Migogoro ya Bima Magreti Mngumi wakati akifanya mazungumzo na mwandishi wa habari hizi katika maonesho ya huduma za kifedha yanayoendelea katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.

Mngumi amesema kuwa lengo la taasisi hiyo ni kutoa huduma za kutatua migogoro ya bima pindi mwananchi anapohitaji kudai fidia ya bima kutokana na madhila waliyoyapata.

‘Hii ni taasisi ambayo inatoa huduma katika utatuzi wa changamoto za wateja wa bima pale ambapo mwananchi kwa namna moja au nyingine anapohitaji kudai fidia ya Bima mfano kwa changamoto ya amepata ajali au chombo chake hivyo iwapo atakutana na  changamoto pindi anadai fidia ni vyema ataka kwetu ili tuweze kumsaidia’amesema Mngumi

Aidha Msajili huyo amewataka kutumia huduma hizo za kibima ili waweze kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maeneo yao.

Amesema ni mahali parahisi kufikika kwa wananchi kwani migogoro mingi wanayoipokea inatokana na wahanga wa ajali wanachopewa ni kidogo ukilinganisha na hasara waliyopata.

‘Nawajulisha wananchi kuwa ofisi hii ipo na serikali imeianzisha kwa ajili yao na pia wiki hii tupo hapa viwanja vya mnazi mmoja kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma za kifedha kitaifa  hivyo wananchi waje kwaajili ya kuwasaidia’ amesema Mngumi

Taasisi hiyo ya serikali ya Ofisi ya Msuluhishi wa migogoro ya Bima imeanzishwa chini ya Sheria ya Bima No.10 mwaka 2009 ikiwa ni njia mbadala wa Mahakama katika utatuzi wa changamoto za wateja wa Bima.

0/Post a Comment/Comments