TCRA YAMFUNGA POLEPOLE MDOMO.

                          

………………….

Kutokana  na ukosefu  wa  Maadili  na weledi wa Utangazaji  kamati ya maudhui ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  imekifungia  kipindi cha Shule ya Uongozi kinachotolewa  kupitia Televisheni ya mtandaoni ya Hamphrey Polepole.

Mbali na kufungiwa kwa kipindi hicho Kamati ya Maudhui TCRA  pia imetoa onyo kali kwa  televisheni hiyo ya mtandaoni inayomilikiwa  na  Mbunge  wa  Kuteuliwa  wa CCM   Hamphrey  Polepole, Uamuzi   huo  umetolewa  leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti  wa  Kamati  ya  Maudhui  ya  Mamlaka  ya  Mawasiliano (TCRA) Habi  Gunze.

Mwenyekiti  huyo  wa  maudhui  TCRA  Habi  Gunze amesema  Kituo  hicho  kimekuwa  kikibadili  aina  ya  maudhui  yake  na kuwa  kipindi  cha  shule  ya uongozi  ambapo  amesema kipindi  hicho  kimekuwa  kikijadili  masuala  ya  uongozi  wa kisiasa nchini  pasipo kuzingatia  sheria kanuni  na maadili  ya  uandishi  na utangazaji wa habari.

Aidha  Gunze  amesema  Kamati  imebaini  kuwa  Televisheni  ya  Mtandaoni  Hamphrey Polepole imekuwa  na mapungufu  ya kutokuwa  na Wafanyakazi  wenye taaluma ya waandishi  na watangazaji  wa Habari  jambo  linalowapelekea  kukiuka sheria, kanuni, msingi na maadili ya uandishi na utangazaji wa habari  katika  kazi zao kitendo  kinachopopelekea  kupotosha umma  na  uchochezi.

Kwa  upande  wake mmiliki  wa Televisheni  hiyo ya  Mtandaoni  Mheshimiwa  Hamphrey  Polepole  amesema amepokea  maamuzi  hayo  ya kamati  huku akiahidi  kukaa  na wasaidizi  wake  na kutafakari  kwa  pamoja  hukumu  hiyo kisha  atatoa  tamko  rasmi.

Maamuzi  ya   hayo  ni  ya  Shauri namba moja la mwaka 2021/2022 dhidi  ya  Televisheni  ya  mtandaoni  ya  Hamphrey  Polepole  inayomilikiwa  na  Mbunge  wa  Kuteuliwa  wa  Chama  cha  Mapinduzi ( CCM )  Hamphrey Polepole  dhidi  ya  mashitaka   ya  ukiukwaji  wa  kanuni  za  Mawasiliano ya  Kieletroniki na Posta  ya  mwaka 2020

0/Post a Comment/Comments