WATANZANIA WATAKIWA KUCHUJA TAARIFA ZITOLEWAZO NA WASIOKUWA WAATAALAMU WA AFYA KUHUSU UVIKO-19.


...........................

NA MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM

Watanzania wametakiwa kuendelea kujikinga na kuchukua tahadhari ya Mawimbi mbalimbali yanayojitokeza ya UVIKO-19 ikiwa ni pamoja na kuchuja taarifa zinazotolewa watu wasiokuwa na utaalamu wa magonjwa hayo.

Hayo yameelezwa leop jijini Dar es salaam na Mtafiti Mwandamizi Taasisi ya Utafiti wa Mgonjwa ya Binadamu (NIMRI) Dkt Kunda John Stephen wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi ambapo amesema licha ya kuwepo na wagonjwa wachache wanaoripotiwa na Wizara ya Afya nchini bado haijafikiwa hatua ya kuita wimbi la nne .

Dkt Stephen amesema kuwa ni vyema wananchi wakasikiliza taarifa zinazotolewa na Serikali kupitia Wizara Husika pamoja na wataalamu walioidhinishwa ili kuepukana na changamoto katika upokeaji wa baadhi ya taarifa kuhusu maradhi hayo.

‘Wananchi wamekuwa wakiitegemea serikali iweze kutoa taarifa kwa kweli kumekuwa na Mawimbi Ya Kwanza,Pili,Tatu na tumesikia kwenye baadhi ya nchi zimeripoti kuwepo na hata hiyo OMICRON wimbi la nne lakini ingawa yote bado hayajafika Tanzania hivyo ni vyema wananchi wakajitahidi kuchuja taarifa wanazozipata hasa wasikilize taarifa kutoka kwa serikali’amesema Dkt Stephen

Kuhusu suala la wananchi kuchanja chanjo ya UVIKO-19,Mtafiti huyo mwandamizi wa NIMRI,amesema serikali imeendelea kuviimarisha vituo vya uchanjaji nchini hivyo amewahamasisha waendelee kujitokeza kwa wingi kwani itawasaidia katika usalama wao.

Amesema kumekuwepo na changamoto ya watu kujisahau kujihadhari na UVIKO-19 lakini pia taarifa potofu zinazotolewa na baadhi ya watu kuhusu ugonjwa huo hivyo amesisitiza juhudi za ziada zinapaswa kuendelea kuchukuliwa ili mawimbi yanayosikika katika mataifa mengine yasije yakaingia nchini.

Katika Hatua nyingine kuelekea sikukuu za mwisho wa Mwaka Krist mass na Mwaka mpya amesisitiza wananchi kuzingatia njia zote za kujikinga wasipate Uviko 19,ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa maji tiririka,kuvaa barakoa,pamoja na kutokushiriki sehemu zenye mikusanyiko.

0/Post a Comment/Comments