SERIKALI YADHAMIRIA MPAKA MEI 2022 WANANCHI WAWE NA ANUANI ZA MAKAZI

Waziri wa Habari ,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye wakati akifungua mafunzo ya utambuzi wa Anuani na Makazi kwa wakuu wa mikoa ,wilaya pamoja na wadau mbalimbali.

................................

NA MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM

Serikali imedhamiria kuwa mpaka kufika Mwezi Mei mwaka huu kila mwananchi awe na anuani ya makazi ili kuisaidia serikali iweze kupanga mipango yake ya maendeleo kwa urahisi.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Habari ,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye wakati akifungua mafunzo ya utambuzi wa Anuani na Makazi kwa wakuu wa mikoa ,wilaya pamoja na wadau mbalimbali.

Waziri Nape amesema kuwa  anuani ya Makazi inatija kiuchumi katika mipango mbalimbali ya kimaendeleo ikiwa ni pamoja na kuwezesha mtu kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa haraka.

Amesema serikali itaendelea kutoa mafunzo kwa wataalamu wa Halmashauri ili kuhakikisha kuwa utaalamu utakaopatikana uweze utekelezaji wa mfumo katika maeneo mbalimbali nchini.

‘Mpaka sasa uwekaji wa miundombinu ya mfumo wa Anuani za Makazi katika Mkoa wa Dar es salaam umefanyika katika Kata  46 kati ya Kata 102  ambapo jumla ya nguzo 2217 zenye mbawa za Majina ya barabara zimesimikwa na vibawa 46,741 vya namba za Nyumba vimebandikwa’amesema Waziri Nape

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makala amesema watahakikisha wanahamasisha suala ya Anuani ya Makazi kuanzia ngazi za mabalozi katika mitaa jambo litakalosaidia wananchi wengi kupata uelewa wa anuani hizo.

‘Kuwa na anuani za makazi ina faida kubwa hivyo tunalipokea kwa furaha na kwa umoja wetu tutahakikisha elimu itawafikiwa wana Dar es salaam wote kwa kujua faida nyingi zaidi za kujua umuhimu wa Anuani za Makazi katika mkoa huu na Tanzania kwa ujumla’amesma RC Makala

Naye Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Macrice Mbodo amesema wameamua kuanzisha huduma hiyo Anuani ya Makazi kwa lengo la kusaidia kurahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo huduma ya Posta Mtandao Mlangoni.

0/Post a Comment/Comments