Mkuu
wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru Mkoa wa Temeke Christopher Myava akizungumza na waandishi wa
habari jijini Dar es salaam (hawapo pichani)
...........................
NA
MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru Mkoa wa Temeke jijini Dar es salaam imewaomba viongozi wa
dini katika nyumba zao za ibada kutumia nafasi ya mahubiri kukemea vitendo vya
Rushwa ili jamii iweze kukidhi katika maadili yasiyokuwa na Rushwa.
Hayo
yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa TAKUKURU (M) Temeke Christopher Myava wakati akizungumza na
wanahabari akitoa taarifa ya kipindi cha miezi mitatu kuanzi mwezi Octoba mosi
mpaka 31/12 mwaka jana.
Myava
amesema kuwa katika kipindi hicho wameweza kupokea jumla ya malalamiko mia moja
na hamsini na tano ambapo kati ya hayo malalamiko 96 yamehusu Rushwa na 59
yalikuwa hayahusiani na rushwa .
Myava amesema wameanza uchunguzi wa malalamiko 96 yanayohusu rushwa, huku majalada 7 uchunguzi wake ukiwa umekamilika, 11 yamefungwa kwa kukosa ushahidi na 78 uchunguzi wake unaendelea.
‘Jumla ya mashauri 22 yanaendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Mkoa wa
Temeke’amesema Myava
Aidha
Mkuu huyo wa TAKUKURU Temeke amevitaja vipaumbele katika kipindi cha Januari
–Machi mwaka huu ambapo amesema watahakikisha wanaongeza kasi ya ufuatiliaji wa
miradi ya maendeleo ili kuziba mianya hasa katika ujenzi wa miradi ya maendeleo ambayo serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi.
Amesema kuwa TAKUKURU Mkoa wa Temeke wanaendelea kutoa elimiu kupitia Makundi mbalimbali yenye kuhamasisha wananchi ili kuongeza uelewa katika mapambano dhidi ya rushwa.
Katika
hatua nyingine Myava amewaomba viongozi wa dini kuendelea kukemea vitendo vya
Rushwa katika nyumba zao za ibada kwani kutoa au kupoka Rushwa imekemewa hata
katika vitabu vitakatifu.
Hata hivyo Mkuu huyo wa TAKUKURU amewakumbusha wananchi kuwa ni vyema wakatanguliza mbele maslahi ya nchi na kuchukua hatua madhubuti katika kukabiliana na tatizo la Rushwa katika mkoa huo kwani ni adui wa haki na inaweza kuathiri mgawanyo wa rasilimali katika jamii.
Post a Comment