Makamu
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais
Zanzibar Othman Masoud akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam
akieleza dhamira yake ni kuendelea kusimamia maridhiano ya kisiasa
....................................
NA
MUSSA KHALID,DAR ES SALAAM
Chama cha Siasa cha ACT Wazalendo kimewataka
wanachama na viongozi wa wa chama kuendelea kudumisha umoja,upendo na
mshikamano katika kujenga Chama mbadala katika kuongoza nchi kwani watanzania
wanaimani kubwa na chama hicho.
Kauli hiyo
imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Juma Duni
Haji wakati akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku chache baada ya
kuchaguliwa na chama chake kushika wadhifa huo ambapo amesema malengo yao ni
kuhakikisha chama kinajipambanua kwa
siasa za masuala muhimu ya kitaifa ya kisiasa,kiuchumi pamoja na kijamii.
Aidha Mwenyekiti huyo ametaja kipaumbele cha
watakayoyatekeleza kuwa ni pamoja na kusimamia na mageuzi ya uendeshaji wa
chama kisiasa,Tume huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya,kuendesha siasa za masuala na kupigania na kutetea Haki,Umoja na
Maridhiano.
‘Nitashirikiana na Makamu Mwenyekiti Zanzibar
kuhakikisha kuwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar unakuwa wa haki na usawa na
hili litawezekana kupitia kuandikwa kwa katiba mpya ambayo itaipa Zanzibar Mamlaka
yake kamili na kuweka usawa baina ya washirika wawili wa Muungano’amesema Duni
Awali akizungumza Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT
Wazalendo Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Othman Masoud amesema
dhamira yake ni kuendelea kusimamia maridhiano ya kisiasa yaliyoasisiwa na
Mtangulizi wake Maalim Seif Sharif Hamad katika kupigania haki za kijamii,haki
za kisiasa na ustawi wa kiuchumi kwa wananchi wote.
Amesema atahuisha utamaduni wa kukifanya chama kuwa
chemuchemu ya Fikra mbadala kwa kuibua hoja na kuanzisha mijadala ya kitaifa
inayopelekea kuimarishwa kwa sera na sheria mbalimbali za kitaifa zinazogusa
maslahi ya moja kwa moja na wananchi.
‘Kusimamia uwajibikaji wa kitaasisi ambapo kila
kiongozi wa chama wa ngazi yeyote kutoka tawi hadi taifa,watendaji wa chama na
wanachama kwa ujumla wanatimiza wajibu wao kwa mujibu wa katiba,Kanuni na
maelekezo mbalimbali ya chama’amesema Mhe Masoud
Hata hivyo amesema kuwa mambo yanayohitajika baada ya kujiunga na serikali ya umoja wa kitaifa ni pamoja kurejesha imani baina ya wananchi na serikali yao na mfumo mzima wa uendeshaji wa nchi,pia kujenga serikali yenye ufanisi na kuimarisha misingi ya utawala bora na uwajibikaji katika uendeshaji wa serikali.
Post a Comment