Mkurugenzi
wa Makumbusho ya Azimio la Arusha, Dkt Gwakisa Kamatula alipokuwa akingelea
Maadhimosho ya miaka 55 ya Azimio la Arusha
Jengo la Makumbusho ya Azimio la Arusha, ndio sehemu kikao kilicho asisi Azimio hilo kilipofanyika
Manara wa kumbukumbu ya Azimio la Arusha, Jijini Arusha
Bango
linalo linaloelezea maadhimisho hayo.
............................
Na Sixmund Begashe
Vijana na wananchi mbalimbali nchini
wameshauriwa kwenda Makumbusho ya Azimio la Arusha kujifunza misingi muhimu
iliyowekwa na waasisi wa nchi hii wakiongozwa na Hayati Baba wa Taifa Mwl Julia
Nyerere 1967.
Wito huo umetolewa na
Mkurugenzi wa Makumbusho ya Azimio la Arusha Dkt Gwakisa Kamatula kwenye
Maadhimisho ya miaka 55 ya Azimio la Arusha yanayoendelea katika Viwanja vya
Makumbusho hiyo iliyopo Jijini Arusha.
Dkt Kamatula amesema kuwa
wameamua kuanzisha maadhimisho hayo ili kupanua wigo wa kutoa elimu na
kuirithisha jamii urithi adhimu wa Azimio la Arusha hasa kwa kizazi cha sasa
ambacho hakina uwelewa mpana kuhusu misingi imara ya nchi iliyosimikwa kupitia
Azimio hilo.
" Waasisi wa
Taifa letu chini ya Hayati Baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere, baada ya Uhuru
walikutana Arusha na kuweka misingi imara iliyosaidia na inaendelea kusaidia
kusukuma maendeleo ya nchi misingi hiyo ni kama vile Umoja wa Kitaifa,
Uwajibikaji, Udugu na Umoja, Utu, Uchapaji kazi kwa faida ya wote nk"
Dkt Kamatula
Naye Mratibu masaidizi wa
Maadhimisho hayo Bi Elizabeth Solomoni amesema maadhimisho ya Mwaka huu
yamehusisha Mada na Maonesho ya Vitu halisia vilivyotumika katika Mkutano wa
Azimio, Majadiliano, wajasiriamali na burudani ya sanaa mbalimbali.
Wakazi mbalimbali
waliotembelea kwenye Maadhimisho hayo akiwepo Bw Juma Kombo mkazi wa Babati
wameipongeza Makumbusho ya Taifa kupitia kituo cha Makumbusho ya Azimio la
Arusha kwa hatua iliyoichukuwa ya kuanzisha Tamasha la Azimio la Arusha kwani
kupitia Tamasha hilo watu wengi watakuwa na hufahamu mkubwa wa umuhimu wa
kuishi katika misingi ya Azimio hilo.
" Watoto wetu
wengi hawana ufahamu kabisa juu ya Misingi iliyowekwa katika Azimio hili,
wamekuwa wakifuata misingi ya nchi zingine, wengi wamejaa ubinafsi, wengine
wanawauwa hadi wazazi wao hawana Utu, heshma imepungua, lakini kwa njia hii
hakika sisi wazazi tunapata matumaini' Mzee Juma Kombo
Tamasha limeanza tarehe 1 Feb 2022. na litafungwa na kuzindua miradi ya ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 inayotekelezwa katika vituo vya Azimio la Arusha na Elimu viumbe, Jijini Arusha.
Post a Comment