Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya JATU PLC Mohamed Simbano wakati akizungumza na waandishi wa habari walipoingia makubaliano ya kumteua Msanii Mrisho Mpoto kuwa balozi kwa miaka mitatu
Mrisho Mpoto ambaye aliyeteuliwa na waziri wa Maji Jumaa kuwa balozi wa
Sekta ya Maji akizungumza mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam
............................
NA MUSSA KHALID
Serikali imeombwa kutambua mchango wa wadau binafsi katika kukuza na
kuendeleza sekta ya kilimo nchini ambayo imekuwa ikiongoza katika kutoa ajira
kutokana na rasilimali zinazozalishwa kutumika kwa ajili ya shughuli za
biashara pamoja na kilimo.
Hayo yameelezwa leo Jijini Dar es
Salaam na Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya JATU PLC Mohamed Simbano
wakati wakiingia makubaliano ya kumteua
Msanii Mrisho Mpoto kwa kuwa
balozi kwa miaka mitatu ili kutangaza sekta ya maji ambayo inaendana
sambamba na kilimo cha kisasa.
Mohammed Simbano amesema Jatu Plc katika kuunga
mkono jitihada za serikali katika kutekeleza na kuendeleza miradi ya
maendeleo ya serekali, Kampuni hiyo imekuwa ikitoa
kipaimbele katika na sekta ya maji kwa kuwa ndiyo nguzo
muhimu katika kilimo cha kisasa.
Aidha Simbano amesema kupitia utaratibu uliopo katika
taasisi hiyo, wameweka njia nzuri za kumuwezesha kila mkulima kumiliki ardhi na
kuwa na matumizi bora ya ardhi huku wakiiomba Serikali
kuishika mkono Jatu Plc kwa kuchochochea maendeleo ya
Taifa kwa kulipa kodi mbali mbali.
Kwa upande wake Mrisho Mpoto ambaye aliyeteuliwa na waziri wa Maji Jumaa
kuwa balozi wa Sekta ya Maji amewaomba watanzania kuendelea kujituma kwa
kufanya kazi kwa bidii ili kumuunga mkono Rais Samia
Suluhu Hassan katika kuwaletea maendeleo wananchi.
‘Lengo langu ni kuhakikisha naendelea kuonyesha ushirikiano kwa serikali
katika utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo ambapo nitaendelea kuzungumza
kuhusu yanayotekelezwa na serikali hivyo natoa fursa kwa wadau mbalimbali
kuunga mkono suala hilo’amesema Mpoto
Mrisho Mpoto ameteuliwa kwa mara nyingine kuwa Balozi wa JATU PLC kwa kipindi kingine cha miaka mitatu ili kuendelea kutangaza miradi mbambali inayofanywa chini ya Rais Samia Suluhu Hassan hasa miradi ya maji na kilimo ili kukuza uchumi wa Taifa na mwananchi mmoja mmoja.
Post a Comment