Taasisi za kidini nchini zimetakiwa
kujitokeza na kumuunga mkono Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan katika Mapambano ya Uviko -
19 .
Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es
Salaam wakati wa uzinduzi wa
Mashindano ya Qaswida zenye tungo zinazohusu Corona
ikiwa ni pamoja na kuchanja pamoja na
kuchukua tahadhari zake nyingine.
Akizungumza katika Uzinduzi huo Mganga
mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Rashid
Mfaume amesema Kupitia tungo hizo za Qaswida
zitasaidia kufikisha ujumbe kwa jamii
na kuelimisha jamii ya Kitanzania katika
kuchukua tahadhari ya uviko -19 kwa kuchanja.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya
vijana Bakwata taifa Alhaji Muharami Hamisi pembe
amesema mashindano hayo ni maalum mkwa
vijana wenye vipaji vya kuimba ili
waonyeshe vipaji huku wakihamasisha jamii
kujilinda na kuchukua tahadhari dhidi
ugonjwa wa Corona unaosababishwa na vijidudu vya
Covid – 19.
Nae Mwakilishi kutoka shirika la MDH
ambaye ni msimamizi wa Miradi ya MDH
Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Alli Kaduma
amesema wameamua kuwasaidia Baraza la Vijana
katika mashindano hayo kutoka na lengo lao
la kuhamasisha jamii kuchukua tahadhari
kupitia tungo za Qaswida kwa kuwa takwimu
zinaonyesha walio wengi ambao wamelazwa kutokana
na ugonjwa wa Corona ni wale ambao
bado hawajachanja.
Mashindano haya ya Qaswida zenye tungo za Uviko – 19 yamezinduliwa leo Februari 09 ,2022 na fainali zikitarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi wa March mwaka huu ambapo leo washiriki mbali mbali wamejitokeza huku wakighani tungo zilizosheheni maneno ya kuhamasisha watu kuendelea kuchukua tahadhari mbali mbali dhidi ya Uviko – 19.
Post a Comment