SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS)
limewatahadharisha wafanyabiashara bidhaa za chakula zilizofungashwa yakiwemo
mafuta ya kula kuweka ama kuanika kwenye jua kwani kunaweza kuleta madhara
makubwa ya kiafya kwa binadamu.
Ameyasema hayo leo Afisa Uthibiti ubora TBS, Baraka
Mbajije wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Makao Makuu
ya TBS, Ubungo Jijini Dar es Salaam.
Amesema katika uchunguzi waliofanya wamebaini wengi
wao wanaweka bidhaa nje kwenye jua ili wateja waweze kuona, sababu ambayo ni
dhaifu kwani kunaweza kuhatarisha afya ya walaji.
Mbajije amesema kuwa kuweka bidhaa za vyakula nje
kwenye jua inapelekea kuharibu kile chakula na ubora wa hiyo bidhaa unapungua
hata kama bidhaa haijafika muda wake wa matumizi kuisha (Expire date).
Aidha amesema wazalishaji wa mafuta ya kula
huongeza virutubisho vya vitamini A kuhakikisha mtumiaji anatumia mafuta
yaliyobora, hivyo mafua yakiwekwa kwenye jua Vitamini A huondoka kwa haraka
hivyo mtumiaji nakuwa kwenye hatari ya kutumia mafuta yasiyo salama.
Pamoja na hayo amesema chakula kilichopigwa na jua kinapoteza radha yake ya asili kwasababu ya shughuli za kemikali zilizkuwa zimefanyika katika kuandaa hicho chakula pia kuzalisha harufu ambazo hazikutarajiwa.
Post a Comment