Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt Agness Kijazi wakati akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es salaam akitoa taarifa ya mwelekeo wa msimu wa mvua za masika Mwezi Machi mpaka Mei 2022.
Mtaalamu
wa Hali ya Hewa
Rose
Senyagwa akitoa tathmini ya mwenendo wa mvua za vuli kwa kipindi cha Mwezi
Oktoba hadi Disemba mwaka 2021.
.......................................
NA MUSSA KHALID
Mamlaka
ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema
katika kipindi cha Mvua za Masika Mwezi Machi mpaka Mei mwaka huu mvua za
wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi yanayopata
misimu miwili ya mvua kwa mwaka.
Hayo
yamelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirikisho la Hali ya Hewa Duniani (WMO) Dkt Agness Kijazi wakati akizungumza na
wanahabari akitoa taarifa ya mwelekeo wa msimu wa mvua za masika Mwezi Machi
mpaka Mei mwaka huu ambapo amesema
zinatarajiwa kuanza mapema kati ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi
Februari na kuisha mwezi Mei mwaka huu katika maeneo mbalimbali nchini.
Dkt
Kijazi amesema ongezeko la mvua hizo linatarajiwa hasa katika kipindi cha Mwezi
Machi katika maeneo ya pwani ya Kaskazini na Mwezi April kwa maeneo ya nyanda
za juu Kaskazini Mashariki.
‘Msimu
wa mvua za Masika ni mahususi kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki (Mikoa
ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro), pwani ya kaskazini (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro,
mikoa ya Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na
visiwa vya Unguja na Pemba), ukanda wa Ziwa Victoria (Mikoa ya Kagera, Geita,Mwanza,
Shinyanga, Simiyu na Mara) pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma’amesema Dkt
Kijazi
Amesema
katika Ukanda wa Pwani ya Kaskazini: (kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mikoa ya Pwani
(ikijumuisha visiwa vya Mafia), Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja
na Pemba) Mvua zinatarajiwa kuwa za wastani hadi juu ya wastani na kuanza kati
ya wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Februari, 2022. Mvua hizo zinatarajiwa
kuisha katika wiki ya tatu ya mwezi Mei, 2022.
Aidha
Mkurugenzi huyo amezitaja athari zinazoweza kujitokeza wakati wa mvua hizo
kwenye sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na usalama wa chakula kuwa vipindi vya
unyevu wa kuzidi kiasi vinaweza kujitokeza na kuathiri ukuaji a baadhi ya mazao
yasiyohitaji maji mengi.
‘Katika
sekta ya Afya Kutokana na mvua zinazotarajiwa, upo uwezekano wa kuongezeka kwa
athari za magonjwa ya kuambukiza, hususan magonjwa yatokanayo na wadudu-dhurifu
na matumizi ya maji yasiyo salama kwa afya. Hivyo, mamlaka husika zinashauriwa
kuhakikisha upatikanaji wa dawa za kutosha katika vituo vya kutolea huduma za
afya mapema, kwa kuzingatia uwezekano wa uharibifu wa miundombinu unaoweza
kujitokeza hususan katika vipindi vya mvua kubwa. Jamii inasisitizwa kuchukua
hatua kwa kuhakikisha usafi wa mazingira yanayowazunguka, kuharibu mazalia ya mbu,
kudumisha usafi kwa ujumla’ameendelea Dkt Kijazi
Awali
akitoa tathmini ya mwenendo wa mvua za vuli kwa kipindi cha Mwezi Oktoba hadi
Disemba mwaka 2021Mtaalamu
wa Hali ya Hewa Rose
Senyagwa amesema kuwa TMA ilitoa utabiri wa uwepo wa mvua za wastani hadi chini
ya wastani ambapo kiwango cha usahihi wa utabiri kilikuwa cha asilimia 93.8.
Hata hivyo Mamlaka hiyo imewashauri watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na wakulima,wafugaji,mamlaka za wanyamapori,wasafirishaji,mamlaka za maji na afya kuendelea kutafuta,kupata na kuzingatia ushauri wa wataalamu katika sekta husika.
Post a Comment