Shirika la Viwango Tanzania –TBS limesema limeanzisha kituo cha Taarifa kwa bidhaa zinazosafirishwa kwenda mataifa mbalimbali ili kutoa usaidizi kwa wafanyabiashara kusafirisha bidhaa zilizokidhi viwango vya nchi husika.
Hayo yameelezwa jijini Dar es salaam na Afisa
Udhibiti Ubora (TBS) Hassan Juma wakati akizungumza na wanahabari akielezea
huduma inayotolewa na TBS ikiwemo ya kutoa ushauri kwa wasafirishaji wa bidhaa
kwenda nje ya nchi.
Hassan amesema kwa nchi za Jumuiya ya Afrika
mashariki bidhaa ambayo imethibitishwa na TBS huwa haina kipingamizi lakini
zinazokwenda nje huwa wanazikagua kabla ya kwenda nje sambamba na utoaji wa
cheti.
‘Kwa bidhaa zinazokwenda nje ya jumuiya ya Afrika
Mashariki huwa tunawapa taarifa ya bidhaa zinavyokwenda huwa tunakagua ubora
wake kabla ya kuisafirisha na pia itatolewa cheti cha uthibiti’amesema Hassan
Kwa upande wake Ibrahim Feruzi kutoka kitengo cha
Upimaji wa Sampuli kwa Hiari (TT)
ameelezea umuhimu wa kulitumia dawati la TT kuwa ni pamoja na kufanya uhakiki wa bidhaa
kwa wajasiriamali wanaoanza biashara kujihakikishia wanapata leseni baada ya
kujihakikishia ubora wa bidhaa zao.
‘Upimaji wa hiari unasaidia wanaohitaji huduma za
upimaji kuhakiki ubora wa bidhaa wanazokuja kuzipima kwa kuhakikisha uimara wa
miundombinu ya miradi mikubwa ya kimkakati lakini usalama kwa ajili ya
watumiaji’amesema Feruzi
Aidha ametoa wito kwa wananchi wote kufahamu kwamba
TBS kuna dawati la upimaji wa sampuli kwa hiari hivyo wanauhuru wa fursa ya
kulitumia dawati hilo kwa manufaa yao kujihakikisha ubora wa bidhaa wanazonunua
na wanazotarati kwenda kuzitumia katika ujenzi na matumizi ya kila siku.
Hata hivyo Feruzi amesema ripoti za wateja ambazo wanazipokea katika dawati lao zinatoka ndani ya siku 7 hadi 14 ikitegemeana na aina ya sampuli na maabara inapopelekwa .
Post a Comment