ITEL TANZANIA YAWATAKA WADAU WA ELIMU KUCHAGIA MAENDELEO YA ELIMU NCHINI.





...............................

NA SALYM BITCHUKA.

Kampuni  ya  Itel  Tanzania  imewataka  Wadau wa elimu nchini kuhamasika  kuunga mkono jitihada za serikali katika kuchangia maendeleo ya elimu nchini

Kauli hiyo  imetolewa  jijini Dar es Salaam wakati kampuni  hiyo ya Itel Tanzania ilipokabidhi msaada vifaa vya shule kwa wanafunzi  wanaotoka katika mazingira magumu  au famili zenye kipato cha chini ya mstari wanaosoma katika shule ya msingi Ubungo NHC jijini hapa kupitia kampeni yao ya CSR.

Akizungumza katika makabidhiano hayo meneja mahusiano Itel Tanzania Fernando Wolle amesema kwa kutambua   watoto ni hazina ya taifa lijalo hivyo itel kwa kutumia kauli mbiu yao ya "Enjoy Better Life" Wanahakikisha wanatengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya kutimiza azma ya kuwasaidia watoto kufurahia maisha bora.

‘Pia tumeanzisha mradi wa maktaba unaojulikana kama ‘Wandering Libraries Project’tangu 2021 na huu utakuwa mradi wa muda mrefu wa CSR wa Itel lengo ni kuchangia maktaba ndogo zaidi ya 10,000 kote barani Afrika katika miaka 3 ijayo.’amesema Wolle

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Ubungo NHC Paulo Mdachi  ameshukuru Kampuni ya Itel Tanzani  kwa msaada huo huku akiwataka wadau wengine wa elimu juiga mfano wa  Itel mobile limited.

Msaada huo uliotolewa  na Kampuni ya  Itel Tanzani kwa wanafunzi  hao  ni pamoja vitabu vya kiada 217 kwa masomo ya sayansi, Hesabu na Kiingereza kwa darasa la tatu la nne na la tano, Shelfu ishirini, Kalamu na mabegi ya shule vikiwa na thamani ya shilingi milioni tano.

0/Post a Comment/Comments