DC GONDWE ATOA TAHADHARI KWA WAMILIKI WA BAR NA KLABU


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe akitolea tamko malalamiko yaliyowasilishwa ofisini kwake na wakazi wa Nzasa kuhusu adha wanayoipata kuhusu kelele zinazozalishwa na muziki katika bar na Klabu.


Mwenyekiti wa mtaa wa Chuo kikuu Nzasa Dkt. Edwinus Lyaya akielezea adha wanayoipata kutokana na baadhi ua klabu na bar zilizopo katika maeneo yao
..........................

Mkuu  wa  wilaya  ya  Kinondoni  Jijini  Dar es  Salaam Godwin  Gondwe  amewataka  wamiliki  wa  Bar  na  Klabu  kuendesha  biashara  zao  kwa  kufuata  sheria, Taratibu , Kanuni  na  Miongozi  na  kuachana  na  kero  ya  kuzalisha  Kelele  kupita  Kiwango.

Hayo  yanajiri  mara  baada  ya  Wakazi  wa  Kata  ya  Kijitonyama  jijini   hapa  kuwasilisha  malalamiko  yao   kwa   mkuu  huyo  wa  Wilaya  kuhusu  baadhi  ya  Bar  na Klabu  kuzalisha  Kelele  zinazotokana  na upigwaji  wa  Muziki kwa  sauti  ya  juu  pamoja  vitendo  vya  utovu  wa  nidhamu  kwa  baadhi  ya  wateja  maeneo hayo.

Akizungumzia  malalamiko  hayo Ijumaa Mei 13, 2022 Mkuu  wa  Wilaya  Godwin  Gondwe  amekiri  kuwepo  kwa   tatizo la  Upigwaji  wa   Muziki  bila  kufuata  sheria  zilizopo  huku akiahidi  kuanzisha  operesheni  maalum  itakayoendana  na utolewa  wa  elimu  kwa  Wananchi  na  Wamiliki wa  Bar  na Klabu  ili  kuondokana  na  adha  hiyo. 

"Hili ni suala ambalo lipo na lazima tukae na tuone ni kwa namna gani tunaweza kulimaliza ila ni lazima wamiliki wa Klabu na bar wasizidishe kupiga muziki zaidi ya desibeli 40 na siku za kazi wafunge saa tano kama vibali vyao vinavyowataka"amesema dc Godwin Gondwe.

Kwa  upande  wao  baadhi  ya  wakazi  wa  eneo  hilo la Kijitonyama  akiwemo  mjumbe  wa  nyumba  Hamsini  Mariam  Sepetu  pamoja  na  Mwenyekiti  wa  Mtaa  wa  Chuo Kikuu  Nzasa  Dkt  Edwinus   Lyaya  wamesema   kwa  pamoja  wamesema  wamekuwa  wakikumbana  na  adha  kubwa   katika   makazi  hayo  ikiwemo  kelele  zinazosababishwa  na  Muziki ,utovu  wa nidhamu  kwa  wateja  wa  maeneo  hayo ya starehe  huku  wakitaka  kuwekwe  taratibu  za  kudumu katika  kudhibiti  hilo.

"Kiukweli hatuchukii wafanyabiashra ila Wateja wao na upiigaji wa muziki kwa sauti kubwa, wanapaki magari hadi kwenye mageti yetu,kondomu chupi zikulitupwa hovyo yaani imekuwa imekuwa ni kero iliyopitiliza" amesema Mariam Sepetu.

Imeelezwa   kuwa  Katika   Vilabu  na  Bar  vilivyopo maeneo  ya  Wilaya   ya   Kinondoni  vimekuwa  havifuati  sheria   za  kuzingatia   upigwaji  wa muziki kwa  nyakati zote.

0/Post a Comment/Comments