Mkurugenzi
Kampuni ya mchongo, Julias Wambogo (kulia) akiwa na Fayaz Diamond Valli Mkurugenzi wa Tech Advisor na Mshauri ufundi wa Kampuni ya Mchongoo (kushoto) wakizungumza na waandish
wa habari kuhusu uzinduzi wa Website ya
Mchongoo.
........................
NA SALYM BITCHUKA
Katika kuhakikisha vijana wa Kitanzania wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na tatizo la ukosefu wa Ajira, Kampuni ya mchongoo ltd imeanzisha jukwaa la kuwasaidia watanzania wenye ujuzi.
Haya yamebainishwa Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Kampuni ya mchongo, Julias Wambogo wakati akizungumza na waandish wa habari kuhusu uzinduzi wa Website ya Mchongoo ambao itakuwa na jukumu la watu mbalimbali wenye ujuzi kujitangaza.
Wambogo amesema sababu iliyomtuma kuanzisha Website hiyo ni baada ya kuona vijana wengi wa kitanzania wakihangaika kwa kukosa fursa huku wakiwa na ujuzi mbalimbali.
'' watu wote wenye ujuzi wa fani mbalimbali wanaruhusisiwa kuainsha kazi zao wanazofanya na website hii itawawezesha kuonekene kwa urahisi zaidi" amesema Julias Wabongo.
Aidha,Wambogo amewataka vijana kuchangamkia fursa hyo kwa kwa jiunga na Mchongoo Website pamoja makampuni mbalimbali kujitokeza kutumia jukwaa hilo ili kujipatia wataalamu mbalimbali.


Post a Comment