Na Mwandishi wetu
Wafanyakazi na wadau wote wa bima nchini wameombwa kuunga mkono jitihada zinazoendelea kufanywa na banki ya Kcb katika kuongeza uelewa na upatikanaji rahisi wa bima kwa watanzania wote
Akizungumza mapema leo jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya uzinduzi wa bima kwa Bank ya KCB, mkuu wa idara ya wateja wa rejareja ,wadogo na wakati, wa bank hiyo Abdul Juma amesema kuwa kupitia Benki Kuu ya Tanzania na Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) wamepewa rasm mamlaka ya kutoa huduma za bima kutoka bank kwenda kwa mteja hivyo kuanzia sasa watu wote wanaweza pata huduma hiyo hata kwa mkopo wa kulipa kidogo kidogo.
Aidha Huduma za Bima za KCB zitakuwa katika makundi tofauti kama vile bima ya maisha pamoja, bima za magari, za vikundi na nyinginezo.
Kwa upande wake mkuu idara ya masoko na mawasiliano ,KCB BANK Christine Manyenye amesema kuwa uzinduzi wa huduma hiyo ni mwendelezo wa ubunifu na kuangalia mahitaji ya wateja wao.
Utambulisho wa Huduma za Bima za KCB unakuwa ni muendelezo wa huduma nzuri na zenye viwango kutoka KCB bank.
Post a Comment