NESI msaidizi anayehudumu katika Zahanati ya Kariakoo (Kariakoo Dispensary) iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Bw. Salum Shabani Mpangula (54) amekamatwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) akiwa na kilogramu 174.77 za dawa za kulevya aina ya heroine nyumbani kwake.
Hayo yamesemwa leo Juni 3, 2022 na Kamishana Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Gerald Kusaya wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam wakati akielezea mafanikio waliyoyapata katika kipindi cha Januari hadi Mei,2022.
Amesema kuwa, mtuhumiwa alikamatiwa nyumbani kwake eneo la Tabata Relini lililopo Halamshauri ya Wilaya ya Ilala jiini Dar es Salaam.
"Mei 12, 2022 katika eneo la Tabata Relini Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ilikamata kilogramu 174.77 za dawa za kulevya aina ya heroine.

Post a Comment