RAIS SAMIA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI JULY 7/2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe.Amos Makalla akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 29,2022 katika Ofisi za Habari Maelezo JNICC Jijini Dar es Salaam. kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu

........................................

NA MUSSA KHALID

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani yatakayofanyika Julai 7 mwaka huu.

Imeelezwa kuwa maadhimisho hayo ambayo yatafanyika kwa mara ya kwanza Dunia, Julai 06 yatatanguliwa na kongamano la mchango wa lugha ya Kiswahili katika harakati za ukombozi wa bara la Afrika likihusisha Viongozi kutoka ndani na nje ya Nchi.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amosi Makala wakati akitoa taarifa ya Mkoa huo kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo kuandaa tamasha la utamaduni la kwanza kitaifa pamoja na siku ya Kiswahili Duniani.

Aidha RC Makalla amesema Julai 04 Kutakuwa na maandamano ya Amani kuhusu Lugha ya Kiswahili na Utoaji haki kutoka Temeke mwisho mpaka Uwanja wa Uhuru ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Katiba na sheria Dkt. Damas Ndumbaro.

Awali Mkuu Mkoa Makala amesema kuanzia Julai 1-3 mwaka huu Wizara ya utamaduni,Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeandaa tamasha la utamaduni la kwanza kitaifa ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa.

‘Julai 03 kutakuwa na Usiku wa Taarabu katika ufukwe wa Coco Beach ukihusisha burudani ya Mziki mwanana kutoka kwa wasanii mbalimbali akiwemo Khadija Kopa, Isha Mashauzi, Patricia Hilary, Mzee Yusuph na wasanii na vikundi ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge Dkt.Tulia Ackson’amesema RC MAKALA

RC Makala amesema kuwa kuandaliwa kwa tamasha hilo ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluh Hassn aliyoyatoa mkoani Mwanza  Septemba 8,2021 katika tamasha la utamaduni ambapo aliagiza ‘Matamasha hayo yafanyike kwa mzunguko kila mkoa ili watanzania waweze kujua mila na desturi za kila mkoa na kila pembe ya Tanzania.

Tamasha hilo litakwenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘Utamaduni wetu,Fahari yetu,tujiandae kuhesabiwa kazi iendelee’hivyo watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi ili kutambua,kuthamini,na kuendeleza urithi wao

0/Post a Comment/Comments