KAMATI KUU CCM YAITAKA SERIKALI KUSIKILIZA MAONI YA WANANCHI KUHUSU TOZO


............................

NA SALIM BITCHUKA,DAR ES SALAAM

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya   Chama  cha  Mapinduzi  (CCM) Taifa imeielekeza  Serikali  kutazama  hali  halisi  na  kuchukua  hatua  stahiki kuhusu  ushauri  na  maoni  ya  wananchi  kuhusu  Tozo   za miamala  ya Kieletroniki, iliyoanza  kutekelezwa  hivi  karibuni.

Kauli  hiyo  imetolewa  leo  jijini  Dar es Salaam  na Katibu wa Halmashauri Kuu  ya  CCM Taifa - Itikadi na Uenezi  Shaka  Hamdu  Shaka   wakati   akiwasilisha  taarifa  kwa  wanahabari  yale  yaliyopokelewa  na  kujadiliwa  katika  kikao  maalum cha Kamati  hiyo  kilichoketi  Septemba saba  mwaka  huu  2022.

Shaka  Hamdu  Shaka  amesema Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imepokea, kutafakari na kujadili kwa kina kuhusu hatua za kibajeti zinazoendelea kuchukuliwa kwa lengo la kupata fedha za kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kasi ili kuwawekea wananchi mazingira mazuri ya kujipatia maendeleo, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025.

Aidha Kamati Kuu imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Samia Suluhu Hassan, kwa  namna  anavyoimarisha huduma za kijamii, kuimarisha ustawi wa wananchi, kukuza uchumi wa nchi na mwananchi mmoja mmoja ikiwa ni pamoja na kutoa kipaumbele katika  Sekta ya Kilimo kwa kutenga bajeti  ya kiasi cha shilingi bilioni 954 ikiwa ni ongezeko la  asilimia  224% .

Sanjari na hayo Katibu huyo wa Halmashauri Kuu ya  CCM Taifa  ametumia  nafasi  hiyo   kuwataka   watendaji   wote  wa   Serikali kushuka  chini  na  kuhakikisha  wanasiliza  Kero  za  wananchi  na  kuzitatua   kwani  serikali   ya  awamu  ya sita  haitokubali  kuwa  na watendaji amabao hawajui  majukumu  yao.

Aidha, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imepokea, kutafakari na kujadili kwa kina kuhusu hatua za kibajeti zinazoendelea kuchukuliwa kwa lengo la kupata fedha za kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kasi ili kuwawekea wananchi mazingira mazuri ya kujipatia maendeleo, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020-2025.

Eneo moja wapo ikiwa ni kupitia Tozo ambapo ni ukweli usiopingika kwamba serikali imeweza kufanya mambo makubwa katika kipindi kifupi kwa mfano; kama vile ujenzi wa vituo vya afya 234 na shule mpya za sekondari 214 na maeneo mengine kadhaa ambayo yanagusa maisha ya watanzania ya kila siku.

Hata hivyo baada ya kutafakari na kujadiliana  kwa kina Kamati Kuu imeona umuhimu wa serikali kusikiliza maoni na ushauri wa wananchi kuhusu utekelezaji wa bajeti hiyo, hususani katika eneo la Tozo za miamala ya kielektroniki, iliyoanza kutekelezwa hivi karibuni.

“Kuongeza upatikanaji wa huduma za kifedha kwa gharama nafuu kwa kupanua wigo wa matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma za kifedha ili kuongeza huduma jumuishi za fedha nchini, kuchochea uwekezaji wa ndani na kukidhi mahitaji halisi ya wananchi hususan wa kipato cha chini na waishio vijijini.”amesema Shaka  Hamdu

Kamati Kuu ya CCM imeelekeza Serikali kufikiria na kujielekeza katika kubana matumizi Serikali, kuendelea kujenga mazingira rafiki na wezeshi ili kujenga uchumi imara unaozalisha kwa lengo la kutanua wigo wa kodi pamoja na kubuni vyanzo vipya vya kodi ili kuwa na viwango pamoja na mfumo rafiki wa kodi kwa kila mmoja.

0/Post a Comment/Comments