Ujumbe kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka umehudhuria mkutano Mkutano wa 51 wa Baraza la Haki za Binadamu unaendelea Geneva, Uswisi.
Katika mkutano huo Ujumbe wa Tanzania imejipanga kuzungumzia Ajenda ya haki ya Maendeleo kwenye Elimu , Afya, Makazi,Maji Salama na Safi .
Pia Ujumbe utaongelea pia athari za Uviko 19 hasa katika sekta ya Utalii na mikakati madhubuti iliyowekwa ya kudhibiti uchumi dhidi ya janga la Kovid 19, ikiwemo kuhimiza utoaji wa chanjo ya uviko na kutangaza Nchi kupitia Royal Tour, ambayo imeleta matokeo chanya yaliyopelekea watalii kuongezeka kwa kiwango kikubwa mbali na Ajenda hizo pia kutakuwa na vikao vya pembeni.
Mkutano huo wa 51 wa Baraza la Haki za Binadamu Umeanza tarehe 12 Septemba na utaendelea hadi tarehe 7 Oktoba 2022 mbali na ujumbe huo pia tunawakilishwa Balozi Maimuna Tarishi kutoka Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Geneva.

Post a Comment