Serikali kupitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia imeahidi kufufua hali Uandishi
, Uchapaji, Uchapishaji
,Usambazaji na usomaji wa vitabu hasa kazi za waaandishi Bunifu.
Kauli hiyo imetoleewa leo
jijini Dar es Salaam na waziri wa Elimu
Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda wakati wa uzinduazi wa Tuzo ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu.
Waziri Profesa Mkenda amesema ili kuweza kuchochea na kufanikisha Uandishi, Uchapishaji na Usomaji
, wizara
imeahidi kupita bajeti ijayo itatenga fedha kwa
ajili ya kununua na kuvisambaza vitabu vya ithibati ili
viwezwe kusomwa na kuleta hamasa.
Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu Taasisi ya
Elimu Tanzania ( TET )
Dkt. Aneth Komba amesema lengo la tuzo hiyo ni
kukuza sekta ya uandishi na uchapaji nchini na kuongeza hari ya Watanzania kujisomea huku
Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Taifa
ya
Uandishi Bunifu Profesa Penina Mlama akisema jamii yoyote ilyostarabika
huthamini waandishi Bunifu huku akibainisha kuwa
Uandishi Bunifu imetoa
mchango mkubwa katika kukuza Lugha
ya Kiswahili Duniani.
Imeelezwa kuwa kuanzishwa kwa Tuzo hiyo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu ya Taifa ni muhimu kwa maendeleo ya nchi
ikienda sambamba na
kuwatambua kitaifa na kuzawadiwa kwa waandishi mahiri wa uandishi Bunifu
katika nyanja za riwaya na
Ushairi kwa kuanzia huku ikiwa
na lengo la kukuza utamadunu wa Tanzania kujisomea na kuhifadhi historia,
amali na mitazamo bora ya watanzania.
Aidha amesema majaji watapitia maandiko ya kila mshiriki atakayetuma kupitia barua pepe na Zawadi nono Kwa washindi itakuwepo ambapo mshindi wa kwanza atapewa kiasi cha shilingi milioni 10 huku wa pili akipatiwa shilingi milioni 7 na watatu atapewa milioni 5 hivyo Waandishi wote wa vitabu andikeni kazi nzuri na hii itakuwa kila


Post a Comment