Mchambuzi wa Hali ya hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini –TMA
Rose Senyagwa akizungumza kwenye kipindi cha Morning Kiss ya Kiss Fm jijini Dar
es salaam katika mada isemayo kuelekea msimu wa mvua za Vuli mwaka 2022,athari
zipi zinaweza kujitokeza.
................................
NA MUSSA KHALID –KISS FM
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Tanzania –TMA imeendelea kuwasisitiza
wakulima kuhakikisha wanatumia njia za kitaalamu za teknolojia ya kisasa katika
kilimo ili kuendana na mabadiliko ya mifumo ya hali ya hewa katika Msimu wa
mvua za Vuli mwaka huu.
Hayo yameelezwa jijini Dar es salaam na Mtaalamu na Mchambuzi wa Hali ya
hewa kutoka TMA Rose Senyagwa wakati akizungumza kwenye kipindi cha Morning
Kiss ya Kiss Fm katika mada isemayo kuelekea msimu wa mvua za Vuli mwaka
2022,athari zipi zinaweza kujitokeza.
Senyagwa amesema kuwa kutokana na Mvua za Vuli mwaka 2022 kutarajiwa
kuwa za Chini ya Wastani hadi Wastani katika maeneo mengi ni vyema Wakulima wakaendana
na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuepuka kulima kwa mazoea.
‘Kwa
mwaka huu baada ya utabiri kutoka kwamba mvua zitakuwa chache au chini ya
wastani katika maeneo mbalimbali wataalamu wa kilimo kwa kushirikiana na
Mamlaka ya Hali ya hewa wametoa ushauri kwamba wakulima kwa kipindi hiki
watumie utaalamu na waendane na
mabadiliko ya tabia nchi’amesema Senyagwa
Aidha
ameishauri jamii kuwa na tabia ya kuhifadhi chakula na maji kwa uangalifu
katika ngazi ya kaya na taifa ili kuweza kuepukana na changamoto katika msimu
huo.
Aidha
akizungumzia sekta ya maji amesema Upungufu
wa kina cha maji katika mito, mabwawa na hifadhi ya maji ardhini unatarajiwa
hivyo mamlaka husika zimeshauriwa kuwa na mipango madhubuti ya uzalishaji
nishati ya umeme kutoka vyanzo vingine tofauti na maji kama jua, upepo na gesi.
‘Vyanzo
vingi vya maji hutegemea zaidi mvua kuwa inaponyeesha kile kina cha maji
kinaongezeka na maji yanaongezeka ya na kunapokuwa hakuna mvua maji yanatumika
hivyo levo ya maji inazidi kushuka’ameendelea kuelezea Senyagwa
Vilevile
ameikumbusha jamii kuhifadhi maji ili hali inapokuwa mbaya zaidi wanapata
msaada kupitia maji waliyoyahifadhi.
Hata hivyo amewashauri watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ikiwa ni pamoja na wakulima, wafugaji, Mamlaka za Wanyamapori, Mamlaka za Maji na Afya waendelee kutafuta, kupata na kufuata ushauri wa wataalamu katika sekta husika.

Post a Comment