Mkurugenzi wa leseni kutoka Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni ( BRELA) Andrew Mkapa akifungua kikao cha kujadili kupata maoni na mapendekezo ya Mabadiliko ya Sheria ya leseni za Biashara ya mwaka 1972
NA SALIM BITCHUKA
Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na
Biashara kwa kushirikiana na
Wakala wa Usajili wa Biashara na
Leseni ( BRELA) pamoja na Taasisi za Sekta
za Umma wamekutana ili kupata maoni
na mapendekezo ya Mabadiliko
ya Sheria ya leseni za Biashara ya
mwaka 1972.
Akifungua kikao hicho leo Septemba
14,2022 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa
leseni kutoka Wakala wa Usajili wa
Biashara na Leseni ( BRELA) Andrew Mkapa
amesema kupitia kikao hicho
kutawezesha kupatikana mchango utakaofanikisha maboresho
ama marekebisho ya Sheria
ya leseni za Biashara , Sura 208
ambayo imeonekana kupitwa na wakati.
Aidha Andrew Mkapa amesema Sheria
iliyopo kwa sasa haiendani na
mazingira ya wakati huu ambapo
imeonekana kuwepo na mikwamo kadhaa
kutokana na Mabadiliko ya Teknolojia
ya Ufanyaji Biashara huku akitolea
mfano uwepo wa Biashara za Mitandao.
Kwa upande wake Afisa Biashara
kutoka Wizara ya Uwekezaji , Viwanda na
Biashara (WUVB ) Denis Mzamiru amesema
kinachowasukuma kufanya maboresho na
Marekebisho ya sheria hiyo ni
pamoja na kuifanya Sheria kuendana
na Mazingira ya Sasa ya
Ufanyaji Biashara ikienda sambamba na
uwepo wa urahisi na wepesi kwa
wafanyabiashara kupata leseni za Biashara.
Kikao hicho cha Siku tatu pia kitawashirikisha wafanya biashara binafsi kupitia miavuli yao kimeandaliwa na Brela ikiwa ni agizo kutoka kwa Waziri wa Uwekezaji,Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji kutaka kuwepo kwa mchakato wa kuboresha sheria ikienda sanjari na kushirikishwa kwa wadu wanaoitumia sheria hiyo

.jpeg)
Post a Comment