NA SALIM BITCHUKA
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali nchini imetoa mafunzo kwa kundi maalum la watu wenye matatizo ya Kusikia lengo likiwa ni kuwapa uelewa sahihi namna bora ya matumizi sahihi ya Kemikali.
Akifungua mafunzo hayo leo jijini Dar es Salaam Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko amesema wanatoa mafunzo hayo ili kuhakikisha kuwa kundi hilo la watu wenye matatizo ya Kusikia linapata uelewa Sahihi wa huduma zinazotolewa na Mamlaka ya maabara ya Mkemia mkuu wa serikali.
Dkt. Fedelice Mafumiko amesema pamoja na kuwaongezea uelewa sahihi pia mamlaka imewaeleza umuhimu wa Kemikali pamoja kueleza namna gani Kemikali inaweza kuleta madahara kama haikutumika vizuri .
Aidha Mkemi Mkuu wa Serikali amesema kwa kuona umuhimu wa Kundi hilo la watu wenye matatizo ya kutokusikia kabisa na kutokusikia vizuri kutoka Taasisi ya Maendeleo kwa Viziwi Tanzania (TAMAVIKA) ameweka wazi kuwa wataweka utaratibu mzuri wa kuwasajili wale wote wanaohusika na uzalishaji ama kutumika katika huduma za Kemikali ikiwemo Matumizi.
Kwa uapnde wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo kwa Viziwi Tanzania (TAMAVIKA) Kelvin Nyema amesema kupitia mafunzo hayo yatawajengea uwezo na uelewa mzuri kuhusu matumizi sahihi ya Kemikali huku akisema Kemikali ni nzuri kama itatumika kwa usahihi katika matumizi sahihi.
Mafunzo hayo yametolewa kwa watu zaidi ya Sitini wenye matatizo ya kutokusikia kabisa na wale ambao hawasikii vizuri kutoka katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam

Post a Comment