LHRC- NCHI 100 DUNIANI ZAFUTA ADHABU YA KIFO, 27 HAZITEKELEZI ADHABU HIYO

 

Mkurugenzi  mtendaji wa Kituo  cha  sheria  na  haki  za Binadamu (LHRC)  Wakili  Anna  Henga wakati  akizungumza  na  wanahabari kuhusu  maadhimisho  ya  20  ya siku ya Kimataifa  ya  kupinga  adhabu  ya  kifo.
.........................

NA SALYIM BITCHUKA

Wakati   dunia ikiadhimisha  siku  ya kimataifa  ya  kupinga Adhabu  ya kifo, Kituo cha Sheria na haki za  Binadamu  LHRC Kimeitaka  serikali  ya Jamhuri  ya  Muungano  wa Tanania  kufanya marekebisho  ya  sheria ya  kanuni ya  Adhabu ili kuondoa vifungu  vinavyoweka  adhabu  ya  kifo ili kulinda  haki ya  kuishi kwa  kuweka  adhabu  mbadala.

Tamko  hilo  limetolewa leo Octoba  10, 2022  jijini  Dar es Salaam na  Mkurugenzi  mtendaji wa Kituo  cha  sheria  na  haki  za Binadamu (LHRC)  Wakili  Anna  Henga wakati  akizungumza  na  wanahabari kuhusu  maadhimisho  ya  20  ya siku ya Kimataifa  ya  kupinga  adhabu  ya  kifo.

Wakili  Anna  Henga  amesema  Adhabu   ya  Kifo ni  adhabu  inayotweza  utu  wa  mtu  na kuvunja  haki ya  kuishi  kama iliovyoainishwa katika mikataba  ya  kimataifa  na  kikanda ya  Haki za  Binadamu.

Aidha   Wakili  Henga  amesema uwepo  wa  Adhabu  ya  Kifo haufanyi  watu  waogope  kutenda  makosa  badala  yake inaongeza  maumivu  kwa  jamii  hasa kwa  familia  za  wafiwa.

Takwimu  kutoka  Mtandao  wa  kidunia wa Kupinga   Adabu ya Kifo  ambapo LHRC  ni  Mwanachama  zinaonyesha  kuwa kati  ya  Mataifa 192 Duniani   nchi  110  zimefuta  Adhabu  ya  Kifo, nchi  55  zinaadhabu  ya  Kifo  kati  ya  hizo  nchi   27  zimekuwa  haitekelezeki  adhabu  hiyo.

Maadhimisho  ya  siku  ya  Kimataifa  ya  Kupinga Adhabu  ya  Kifo huadhimishwa  kila  ifikapo Octoba  10  ya  kila  mwaka  ambapo  kwa  mwaka huu  yana kauli mbiu  isemayo  “ Adhabu  ya Kifo  barabara iliyojaa  Mateso “

0/Post a Comment/Comments