SALIM
BITCHUKA
Chama
cha Alliance For Democratic Change (ADC) kimewataka watendaji na viongozi wote
kushikana pamoja katika kumsaidi Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha matatizo
ya Watanzania yanaondoka.
Kauli
hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na mwenyekiti taifa wa chama cha ADC,Hamad Rashid wakati
akifungua mkutano wa Bodi ya uongozi Taifa wa chama hicho.
Hamad
Rashid amesema kumekuwa na baadhi ya watendaji wa serikali wakikwamisha baadhi
utekelezaji wa miradi ikiwemo katika eneo la maji,umeme na bei ya Chakula
kushindwa kujibu maoni sahihi ya
ufumbuzi yanayowasilishwa kwao.
Kwa
upande wake katibu Mkuu wa ADC Doyo Hassan Doyo kupitia mkutano huo
ametambulisha mabadiliko ya rangi za chama hicho kutoka blue na kuwa rangi ya chungwa.
Chama
cha Alliance Democratic Change ADC
kimekuwa ni miongoni mwa vyama vyenye usajili wa Kudumu kutoka kwa msajili wa
vyama vya siasa ambapo leo kulikuwa na mkutano Mkuu na wajumbe wa bodi kikijadili ajenda Kumi na moja ambazo
wanatarajibkuzitolea maamuzi.

Post a Comment