RAIS SAMIA ATUMA SALAMAU ZA POLE KAGERA




 ...........

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kufuatia ajali ya ndege ya Kampuni la Ndege ya Precision Air kuanguka katika Ziwa Victoria baada ya kushindwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Bukoba mkoani Kagera.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia ameandika;Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali wa Ndege ya Shirika la Precision katika Ziwa Victoria mkoani Kagera.Natuma salamu za pole kwa wote walioathirika na ajali hii.Tuendelee kuwa watulivu wakati zoezi la uokoaji likiendelea kuhu tukimuomba Mwenyezi Mungu atusaidie.

0/Post a Comment/Comments