Salum
Bitchuka
Imeelezwa
kuwa kundi la watoto ndilo kundi linaloathirika zaidi kuliko makundi mengine
katika mabadiliko tabia nchi hapa nchini
.
Hayo
yameelezwa jijini Dar es Salaam na Afisa Ushauri elekezi kutoka Shirika la
Forum CC Baraka Machumu wakati wa mdahalo wa
kuangalia madhara wanayopata
watoto yanayotokana na mabadiliko tabia nchi.
Baraka
amesema kati ya kundi la wazee na vijana kundi la watoto limekuwa likikosa haki zao za msingi kutokana na mabadiliko
tabia nchi ikiwemo kukosekana elimu bora
,magonjwa na haki ya kucheza.
Kwa
upande wao baadhi ya watoto walioshiriki mdahalo huo wamesema wameweza kupata elimu ya kutosha kuhusu
athari za mabadiliko tabia nchi na wao
wanakuwa mabalozi kuweza kutoa elimu hiyo kwa watoto wenzao.
Shirika
la Forum CC wanatengeneza jukwaa la watoto kuweza kujifunza na kuelewa
mabadiliko tabia nchi na namna gani watoto wanaweza kupaza sauti kuhusu
mabadiliko tabia nchi.
Post a Comment