Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Damu na Mkuu wa Kitengo cha Wagonjwa wa Damu Muhimbili Dkt.Stella Rwezaula akizungumza na waandishi wa habari jana Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam.
Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Dkt.Victor Mgotta akizungumza na waandishi wa habari jana Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam.Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kushirikiana na wataalamu kutoka nchini Kenya kufanya tohara salama kwa wagonjwa 25 wenye changamoto ya uvujaji wa damu (HIMOFILIA).
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Damu na Mkuu wa Kitengo cha Wagonjwa wa Damu Muhimbili Dkt.Stella Rwezaula amesema kuwa kuwa zaidi ya watanzania 5800 wana tatizo la haemophinia bila kujua kuwa wanatatizo hilo.
Aidha Dkt.Stella amewashauri watu kuacha imani za kishirikina, wasiende kwa waganga wa kienyeji pale wanapomuona mgonjwa anayetokwa damu puani, au anayetokwa na damu isivyokawaida aking’olewa jino au baada ya kufanyiwa tohara n.k, bali waende kwa wataalamu wa afya ili wapewe matibabu sahihi.
Naye Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Dkt.Victor Mgotta ametoa wito kwa wanaotokwa na damu bila udhibiti wajitokeze kwenye vituo vya afya vya kanda ili waweze kupatiwa matibabu.
Hoemophibia ni ugonjwa wa kutokwa damu bila ukomo, ambapo imeelezwa kuwa asilimia 70 ya wagonjwa hurithi kutoka kizazi hadi kizazi, na asilimia 30 hupata kutokana na mabadiliko ya vinasaba.


Post a Comment