Na
Mwandishi wetu
Afisa
elimu mwandamizi Mkumbusho ya Taifa Anamery Bageny amewataka Watanzania kuendelea
kujiwekea tabia ya kufanya utalii katika maeneo mbalimbali nchini ili wajifunze
urithi wa nchi yao.
Bageny
amesema hayo jijini Dar es salaam katika ziara maalum ya utalii ya katika
program ya Museum University Hub ambayo imeandaliwa na Makumbusho ya Taifa kwa
kushirikiana na Taasisi ya wanafunzi wanaosoma taaluma ya urithi wa utamaduni
kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Amesema
kuwa jamii imekuwa na mazoea ya kudhani kufanya utalii ni kwenye mbuga za
wanyama maeneo tengefu hivyo ni vyema pia wakajikita katika kufanya utalii wa
kiutamaduni ukiwemo wa jiji.
‘Tunawapa
wanafunzi nafasi ya kulitazama jiji la Dar es salaam kwa jicho la utalii kwa
sababu wamekuwa wakipita katika maeneo hayo wakielekea katika maeneo mbalimbali
kwani Makumbusho tumekuwa tukiifungua Dar es salaam ili kuhakikisha watalii
wanaongezeka kwa wingi’amesema Bageny
Amesema
malengo yao pia ni kuhakikisha wanawaelimisha watanzania kuhusu kufanya utalii
wa kiutamaduni ikiwa ni pamoja na kujifunza urithi uliopo kwenye nchi yao.
Aidha
Bageny amewasisitiza watanzania kuendelea kutoa nafasi kwenye utalii wa
kiutamaduni hasa unaopatikana katika jiji la Dar es salaam ili waendelee kuuza
mji huo.
Bageny
ameyataja baadhi ya maeneo ya kiutalii katika jiji la Dar es salaam kuwa ni
pamoja na Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni,Kijiji cha Makumbusho,Soko la
samaki feri,Mnara wa askari pamoja na Magofu ya Kunduchi.
Naye
Muhifadhi Mkuu Daraja la kwanza Malikale na Kamanda wa Kituo cha Mgofu ya Kale Kunduchi
amezipongeza taasisi mbalimbali kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika
kuhamasisha utalii wa ndani.
Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi na wadau ambao wameshiriki katika kufanya utalii huo wamesema kuwa wamejifunza mambo mengi ya kihistoria hivyo watakuwa wajumbe wa kuishawishi jamii kujifunza na urithi wan chi.



Post a Comment