TBS YATOA KANUNI 5 YA KUHIFADHI CHAKULA SALAMA

Kaimu Meneja Kitengo cha Tathmini ya viatarishi vya Chakula TBS Ashura Katunzi Kilewela akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.

.........................

NA MUSSA KHALID

Shirika la Viwango Tanzania –TBS limewasisitiza watanzania kuzingatia kanuni tano za usafi na ulaji wa chakula salama ili kuweza kuepukana na madhara yanayotokana na kutokula chakula salama.

Pia imeelezwa kuwa ili mwananchi kuwa na chakula toshelevu ni vyema akawa na chakula salama katika kaya ambacho maandalizi yake yanaanzia shambani.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es salaam na Kaimu Meneja Kitengo cha Tathmini ya viatarishi vya Chakula TBS Ashura Katunzi Kilewela ambapo amesema kuwa ni vyema jamii ikazingatia kanuni tano za kuwa na chakula salama ikiwa ni pamoja na kuzingatia usafi.

Aidha ameitaja kanuni nyingine kuwa chakula kinapaswa kupikwa mpaka kiive ili kuondoa uwezekano wa vimelea vya magonjwa kuweza kumdhuru mtumiaji.

‘Tunaposema usafi kwa wakati huu kuna kuwa na maandalizi ili wanakaya waweze kukila hicho chakula kuanzia namna ambavyo unakiosha au vyombo ambavyo unavitumia katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwa mama lishe ni muhimu kuzingatia suala la usafi’amesema Kilewela

Kanuni nyingine amesema ni muhimu kuitenganisha chakula kilichopikwa na kibichi ili kama kunauchafuzi wowote kwenye chakula kibichi au vimelea vya magonjwa isije ikahatarisha kilichopikwa na kukosa usalama.

Wakizungumza na kituo hiki baadhi ya waandaji wa chakula wamesema wamekuwa wakizingatia usafi wa chakula kabla na baada ya kuwapatia walaji jambo huku wakiwashauri waandaaji wengine wa chakula kutokujisahau.

Hata hiyo Kilelewa amesema wataendelea kushirikiana na watendaji wengine kwenye kata wakiwemo maafisa ugani na afya kwa kutoa mafunzo ili elimu ifike na kuhakikisha mlaji anapata chakula kilichobora na salama.

0/Post a Comment/Comments