***************
Na Richard Mrusha Handeni
WATU watatu wa familia ya Mzee Amri Nyundo wa Kijiji cha Kwamwachalima ,kata ya Kwamkonga wilaya ya Handeni mkoani Tanga wamepoteza maisha na watu wengine nane wamejeruhiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya Bombo mkoani humo Kwa ajali ya moto uliotokana na Lori lililobeba gesi kudondoka na kulipuka.
Akithibitisha kutokea Kwa ajali hiyo leo Machi 31 mbele ya waandishi wa Habari mkuu wa Wilaya hiyo Albert Msando Amesema nikweli ajali hiyo imetokea na imesababisha vifo vya watu watatu kutoka familia Moja lakini na watu wengine nane wamejeruhiwa Kwa asilimia 90 na hali zao mbaya sana.
Amesema ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo saa 11 ambapo Lori lililokuwa limebeba gesi kutoka Dar es Salaam na kuelekea Nairobi Kenya,kwakile kilichodaiwa kupasuka taili moja kisha kudondoka na kulipuka kwa moto, kuanza kusambaa kwenye makazi ya watu na kusababisha vifo, majeruhi na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya umeme.
" Kama mnavyoona hapa ndugu waandishi wa Habari hii ni ajali iliyotokana na moto wa gesi ambapo watu watatu wa familia Moja kufariki dunia na Kati yao watoto wawili na mama yao wote wamepoteza maisha."amesema Mkuu wa Wilaya Msando
Nakufafanua kuwa " mama huyo amepoteza maisha akiwa katika harakati za kuwaokoa watoto wake ambao walikuwa wamelala ndani ya nyumba yao. Sisi kama Serikali tumebeba msiba huu na tumekwenda kuzika katika Kijiji cha jirani na majeruhi wote nane wamelazwa katika Hospitali ya Bombo na Serikali inashughulikia matibabu yao."Amesema Msonda
Katika hatua nyingine mkuu wa Wilaya huyo amefafanua kuwa kutokana na ajali hiyo pia imeharibu miundombinu ya umeme ikiwamo nguzo zake kuungua ambapo Tanesco pamoja na vyombo vya Dora wapo katika eneo hilo la tukio kuhakikisha wanarejesha Kwa miundombinu iliyoharibika.
Pia amewashukuru wananchi wa kata hiyo na Kijiji cha kwamwachalima Kwa ushirikiano walioonyesha mara baada ya kutokea Kwa ajali hiyo nakwamba walishirikiana kikamilifu na Jeshi la Zima moto na uokoaji kuhakikisha wanadhibiti Kwa haraka kusambaa Kwa moto huo.
Naye Habiba Omari na Ibrahimu Abdallah ni mashuhuda wa ajali hiyo na wakazi wa Kijiji hicho wamesema kuwa walisikia kishindo kikubwa barabarani baada ya kutoka nje ndipo walipoona Lori kubwa lililokuwa limebeba gesi lilokuwa likitoka Dar es Salaam likiwa limepinduka na kulipuka.
Wamesema kuwa kutoka na ajali hiyo imesababisha vifo hivyo vya watu watatu ambao wote wametoka kwenye familia ya mzee Amri Nyundo ambaye ni Mume wa mama aliyefariki ambapo hata hivyo Yeye yupo safarini Dar es salaam..
Mwisho

Post a Comment