' ''''''''''''''''''''''''''''''''''''''
Serikali Mkoani Dodoma imeendelea kuimarisha miundombinu katika sekta ya Elimu
na Afya kwa lengo la kuboresha na kusogeza huduma kwa wananchi.
Hayo yamebainishwa leo tarehe 02/05/2023 na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma
Bw. Ally Gugu alipofanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Chemba kukagua miradi ya
maendeleo.
Bw. Gugu ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa madarasa, maabara na zahanati katika
Vijiji vya Jangalo, Soya na Ombiri ambapo ujenzi wake uko katika hatua za mwisho
na umegharimu kiasi cha Shilingi millioni 90.6 kwa madarasa 12 na maabara 1, kwa
upande wa ujenzi wa zahanati umegharimu kiasi cha Shilingi millioni 50.
"Ndugu zangu Serikali inatoa fedha nyingi kwa ajili ya kukamilisha miradi hii ya
maendeleo, nitoe rai kwenu kwanza kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati,
pili miradi ikamilike kwa ubora wa hali ya juu” Gugu amesisitiza.
Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Bi. Siwema Jumaa
amesema mbali ya fedha kutoka Serikali kuu utekelezaji wa miradi hiyo ni pamoja na
jitihada za nguvu za wananchi ambao kwa baadhi ya majengo ya zahanati na
madarasa wananchi wamejenga maboma.
Pia, amewataka wakazi wa vijiji vya Jangalo ,Soya na Ombiri kuwa walinzi namba
moja wa miradi hiyo kwa kuwa inaghariimu fedha nyingi za Serikali.
Ziara ya Bw. Gugu ilianzia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wa Chemba na Ofisi ya
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Chemba kuongea na watumishi na
kufanikiwa kukagua umaliziaji wa vyumba vitatu vya madarasa shule ya Msingi
Ombiri, ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa, jengo la Utawala, matundu 30 ya vyoo
katika shule ya Msingi Soya, umaliziaji wa chumba 01 cha maabara shule ya
Sekondari Jangaro na ujenzi wa Zahanati ya Mlongia.
Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Senga Gugu
amefanikiwa kuongea na watumishi na kuwaasa kufanya kazi kwa weledi,
ushirikiano, kupendana na kufanya kazi kwa ubora na kuepuka kufanya kazi kwa
mazoea .



Post a Comment