WANASAIKOLOJIA WATAKIWA KUJIKITA KUJUA KIINI CHA VISABABISHO VYA UKATILI KWENYE JAMII.

Kamishna msaidizi wa Ustawi wa Jamii kutoka  Wizara ya Maendeleo ya Jamii,jinsia wanawake na makundi maalum Baraka Makona wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Mkutano mkuu wa saba wa chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) ambao umekuwa na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili,Ustawi wa Kisaikolojia na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050’uliofanyika leo jijini Dar es salaam.Rais wa Chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) Magolanga Shagembe akizungumza na waandishi wa habari katika Mkutano mkuu wa saba wa chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) ambao umekuwa na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili,Ustawi wa Kisaikolojia na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050’uliofanyika leo jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linalohusika na Malezi na Makuzi ya watoto na utoaji wa huduma ya afya ya akili kwa jamii Tanzania-REPSSI Edwick Mapalala akiwasilisha mada katika Mkutano mkuu wa saba wa chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) ambao umekuwa na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili,Ustawi wa Kisaikolojia na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050’uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano mkuu wa saba wa chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) ambao umekuwa na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili,Ustawi wa Kisaikolojia na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050’uliofanyika leo jijini Dar es salaam (picha na Mussa Khalid)

...................

NA MUSSA KHALID

Wataalamu wa saikolojia nchini wametakiwa kujikita kujua kwa kina chanzo cha visababisho vya matukio ya kikatili yanayoibuka kwenye jamii ili kuweza kuepukana na matukio hayo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Kamishna msaidizi wa Ustawi wa Jamii kutoka  Wizara ya Maendeleo ya Jamii,jinsia wanawake na makundi maalum Baraka Makona wakati akizungumza katika Mkutano mkuu wa saba wa chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) ambao umekuwa na kauli mbiu isemayo ‘Afya ya Akili,Ustawi wa Kisaikolojia na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050’

Makona amesema ili kuwasaidia wananchi kufahamu namna ya kupata huduma ni vyema wataalamu hao wasaikolojia wakawa sehemu ya serikali ili kuishauri  jamii iwezekuishi katika maisha ya furaha.

‘Wananchi wengi bado hawafahamu wapi wapate huduma mbalimbali sababu masuala yote haya ndio yanafanya aishi kuwa na furaha hivyo kama serikali tunataka hawa wataalamu wawe ni sehemu ya serikali katika kuhakikisha kwamba huduma hizi za kuwashauri watu wanazifahamu”amesema Makona

Kwa upande wake Rais wa Chama cha wanasaikolojia Tanzania (TAPA) Magolanga Shagembe amesema kuwa malengo yao ni kuhakikisha wanasimamia elimu kwa jamii ili iweze kutambua uwezo walio nao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kujipatia kipato.

Amesema kuna umuhimu wa kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa na afya nzuri ya akili na ustawi mzuri wa kisaikolojia na kijamii katika kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na hivyokupunguza maovu ambayo yanachangia kukwamisha jitihada za kuweza kufikia malengo yaliyowekwa.

Nao Baadhi ya Washiriki  katika Mkutano huo akiwemo Mkurugenzi Mkazi wa Shirika linalohusika na Malezi na Makuzi ya watoto na utoaji wa huduma ya afya ya akili kwa jamii Tanzania-REPSSI Edwick Mapalala,pamoja na Msaikolojia Anti Sadaka wamesema changamoto ya watu wengi inachangiwa na matatizo ya afya ya akili.

Mkutano huo umehudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa masuala ya saikolojia,maafisa ustawi wa jamii, wanafunzi na viongozi wa kanda.

0/Post a Comment/Comments