..................
Kiongozi wa Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga, ametangaza siku tano za maombolezo kwa wafuasi wake waliokufa wakati wa maandamano ya ghasia yaliyotokea Jumatano, Julai 12.
Kiongozi wa ODM, ambaye alielezea huzuni yake baada ya kifo cha wafuasi waliofariki, alisema kwa siku tano zijazo, muungano utakuwa katika kipindi cha maombolezo, na fikira na sala zao pia zitawaendea wale waliojeruhiwa wakati wa maandamano.
Katika mkutano na waandishi wa habari Raila amesema baada ya siku tano za maombolezo kukamilika, maandamano ya Azimio yataendelea Jumatano, Julai 19.
.jpeg)
Post a Comment