Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kinondoni limewataka wananchi wanaojenga majengo katika mkoa huo kuhakikisha wanazipeleka ramani zao kwa jeshi hili ili kuepukana na changamoto wakati wa uokozi.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mrakibu Mwandamizi na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kinondoni ambao unahudumia Wilaya mbili za Kiserikali Kinondoni na Ubungo Elisa Mugisha wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa ramani.
Mrakibu Mwandamizi Mugisha amesema kuwa ni muhimu ramani kupitishwa kwani kinga na tahadhari ya moto inaanzia katika usanifu wa jengo ili kunapotokea changamoto inayohitaji uokozi wanafanikisha kwa wakati.
‘Hiyo itasaidia kuangalia wakati wakutoka watu wengi watatokaje,milango imekaaje hivyo tunaendelea kuwasisitiza wananchi wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo na Kinondoni wazilete ramani zao za majengo kwani kutofanya hivyo itakuwa wamevunja sheria”amesema Kamanda Mugisha
Aidha amesema kuwa Manispaa ya Ubungo hawana muamko wa kupeleka ramani hizo kama ilivyo kwa Manispaa ya Kinondoni hiyo amewataka kabla ya hatua kuchukuliwa ni vyema wakatekeleza hilo.


Post a Comment