Hayo amesema leo Alhamisi Agosti 3,2023 na Mkurugenzi Mkuu NHC, Hamad Abdallah wakati akizungumza na wahariri na waandishi katika kikao kazi.
Kikao hiko ni mwendelezo wa agizo la Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu aliyezitaka taasisi zote za Serikali kukutana na wahariri na waandishi ili kueleza shughuli wanazozifanya.
Mkurugenzi huyo amesema nyumba hizo 711 ni miongoni mwa miradi ya NHC iliyokuwa imekwama kwa kukosa fedha, lakini sasa Serikali imeliruhusu Shirika hilo kwa kulipatia Sh173.9 bilioni ili kuumaliza mradi huo na ule wa Morocco Square.
Aidha Abdalah amesema NHC itakuwa ikitengeneza Sh850 milioni kila mwezi kutoka katika mradi wwa 'Moroco Square ambapo pesa hiyo itatokana na kodi za wapangaji wa hoteli na maduka huku akidau mradi umekamilika kwa asilimia 97 na tayari umeshapata wapangaji na wanunuzi.

Post a Comment