********
MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma Mariam Ditopile amegawa mitungi 250 ya Taifa gesi ya kupikia kwa Jumuiya ya Wanawake Tanzania( UWT) Wilaya ya Kondoa, lengo likiwa kumtua mama kuni kichwani.
Aidha uamuzi huo wa kugawa mitungi hiyo ni kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ambaye amedhamiria kuondoa nishati chafu ya kupikia kama kuni na mkaa na jamii itumie nishati safi kama gesi ya kupikia.
Mariam amegawa mitungi hiyo leo Oktoba 13, 2023 wilayani Kondoa, wakati akizungumza na wanawake wa UWT ambao wanaadhimisha wiki ya UWT katika Wilaya hiyo.
"Leo tuko hapa katika maadhimisho ya UWT Wilaya ya Kondoa na kila mwaka huwa tufanya wiki ya UWT kuanzia ngazi ya kijiji, kata, wilaya, mkoa mpaka Taifa.



Post a Comment