TMA YATOLEWA UFAFANUZI TAARIFA ILIYOSAMBAA MTANDAONI KUHUSU EL NINO.

.............,......

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa ya tahadhari inayosambaa kuhusu uwepo wa Pacific Elnino na Atlantic El nino hatari sana na kuitaka jamii kununua jiki,water guard kwa ajili ya kuweka kwenye maji ya kunywa pamoja na masuala mengine yaliyoelezwa kwenye ujumbe huo, Aidha, ujumbe huo umekuwa ukisambaa kwenye mitandao ya kijamii na hivyo kuletea taharuki kwa wananchi.

Kwa Mujibu wa Taarifa ambayo imetolewa Leo na Kitengo cha Uhusiano TMA,imesema taarifa hiyo sio sahihi,kwani taarifa sahihi iliyotolewa tarehe 24 Agosti, 2023 kwa vyombo vya habari na Kaimu Mkuruhgenzi Mkuu wa TMA na kutolewa maelekzo na viongozi mbalimbali wanchi sambmba na kusambazwa kupitia vyanzo rasmi vya habari. 

Imesema Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaendelea kusisitiza umma kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na TMA pamoja na ushauri wa kisekta unaotolewa naTaasisi zenye Mamlaka kulingana na sheria na taratibu za nchi.

 Aidha, ikumbukwe kuwa ni kosa kwa mujibu wa sheria Na, 2 ya mwaka 2019 ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kwa mtu yeyote kutoa tahadhari ya hali mbaya ya hewa kinyume na taratibu na bila idhini ya Mamlaka

0/Post a Comment/Comments