..................
Timothy Marko
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imewataka walipa kodi wakubwa kutekeleza matakwa ya kisheria ya ulipaji kodi .
Akizungumza katika kikao kilicho wakutanisha walipakodi wa wakubwa nchini jijini Dar es salaam Kamishina wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA Alphayo kidata amesema sekta ya umma nikichocheo cha maendeleo ya kiuchumi nakuzitakataasisi hizo kulipa kodi zao kwa wakati.
"Uhakika wa wamakusanyo ya kodi katika taasisi za umma na binafsi ndio chanzo cha Mapato ya. Serikali,Mapato haya ndio hutumika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo"Alisema Kamishina Alphayo kidata.
Kamisha kidata alisema Ulipaji wa kodi stahiki nikwamujibu wa sheria ikijumuisha sekta binafsi na uuma.
Alisema Taasisi za Umma ni Muhimu kulipa kodi nasuala hilo ni lazima nasio la hiyari.
"Naziomba taasisiza umma zishirikiane na taasisi za binafs katika kukuza uelewa wa ulipaji kodi".Aliongeza Alphayo kidata.
Katika hatua nyingine Kamishina wa Walipa kodi wa Wakubwa Thomas Muhoja amesema lengo lamkutano huo unalenga kuzungumzia mabadiliko ya kodi ambayo yatatumika katika mwaka ujao wa fedha.
Alisema TRA inawakumbusha walipakodi kutekekeleza magizo ya mamlaka hiyo ilikuweza kuchangia maendeleo ya taifa.
"TRAtuna wakumbusha kutimiza maelekezo ilikuchangia maendeleo ya nchi".Alisema Muhoja.

Post a Comment