WANUFAIKA WA MIKOPO ELIMU YA JUU HAWAJALIPA SH 700 BILIONI


Mkurugenzi Mkuu Wa Bodi ya Mikop ya Elimu ya juu nchini (HESLB), Abdul-Razaq Badru akizungumza  jijini Dar es Salaam, katika kikao kazi kati ya bodi hiyo na wahariri pamoja na waandishi Wa habari. 
Afisa uhusiano na Mawasiliano kutoka Ofisi ya Msajili Wa Hazina, Sabato Kosuri, akiongoza kikao  kazi na kati ya Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu nchini (HESLB), 
na wahariri pamoja na waandishi Wa habari. 




Wahariri pamoja na waandishi Wa habari Wa vyombo mbalimbali hapa nchini wakiendelea na kikao kazi kati yao na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Tanzania na wao



Baadhi ya Viongozi na wafanyakazi Wa Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu nchini (HESLB), wakifuatilia kikao kazi hicho mapema Leo jijini Dar es salaam. 

(PICHA ZOTE NA JAMES SALVATORY) 
********

 Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu nchini (HESLB), imesema, tangu kuanzishwa kwake Ukwasi umefikia zaidi ya shilingi trillioni 7.2 ambazo zimekwenda kwa wanufaika 750,000 nchini. 

Akizungumza jijini Dar es Salaam, katika kikao kazi kati ya bodi hiyo na wahariri pamoja na waandishi Wa habari chini ya utaratibu Wa ofisi ya Msajili Wa Hazina,  Mkurugenzi Mkuu Wa (HESLB), Abdul-Razaq Badru amesema kufikia septemba mwaka huu kiasi cha mikopo ambacho kimekusanywa kinakadiriwa kufikia shilingi trillioni 1.3 kutoka kwa wakopaji  zaidi ya 230,000.

Aidha amesema kiasi cha shilingi billioni 700 cha mikopo hiyo zimeiva lakini hazijakusanywa. 

Pia, amesema wapo katika hatua za kushirikiana na wadau mbalimbali ili  kufanikisha ukusanyaji Wa mikopo hiyo ikiwemo kuunganisha mifumo yao na hifadhi za Jamie na mamlaka ya mapato Tanzania kuendelea kutoa Elimu. 

Amesema kwa sasa mifumo yao imeunganishwa na mifumo mama ya Taifa kwa ajili  ya kuongeza ufanisi na utekelezaji Wa majukumu yao. 

Kwa upande wake afisa uhusiano na Mawasiliano kutoka Ofisi ya Msajili Wa Hazina, Sabato  Kosuri, amesema kuwa wanasimamia maslahi ya serikali kwenye Taasisi za umma.

0/Post a Comment/Comments