BENKI YA MWANGA HAKIKA YAZINDUA PINK AKAUNTI KUMWINUA MWANAMKE KIUCHUMI.

.....................
Timothy Marko 

KATIKA kuhakikisha wanawake wanawezeshwa kiuchumi, Benki ya Mwanga Hakika imezindua Pink Mwanamke Akaunti ilikuweza kumuwezesha kiuchumi.

Akizungumza na waaandishi  wa Habari jijini Dar es salaam Meneja Mwandamizi wa kitengo cha biashara  Judith Halinga amesema kuwa Akaunti ya Mwanamke pink Akaunti haina makato kwa mwanamke katika Benki hiyo.

"Sambamba Pink Akaunti tuna Pink loan hii Mikopo inayomuwezesha kwa mwanamke katika kufanya Biashara na ujenzi wa Nyumba wakinamama "Alisema Meneja Mwandamizi wa Benki ya Mwanga Hakika Benki Judith Halinga.

Judith Halinga alisema Benki hiyo inawawezesha kupatamikopo isiyo nariba kwa mikopo ya Biashara na ujenzi wa nyumba  kwa wanawake.

Alisema sambamba na Mikopo hiyo benki ya Mwanga hakika pia ina huduma ya  Pick Card ambayo inayomuwezesha mwanamke  kufanya manunuzi ya Bidhaa.

"Pia katika Benki yetu tunatoa Elimu ya kuchukua Mikopo yenye tija".Aliongeza Judith Halinga.
 
kwa upande wake Mkurugenzi wa taasisi JSG  Travellers Venancia Msita  amesema  wanawake wajasiliamali kufanya Benki kuwa sehemu Rafiki ilikuweza kukua kibishara.

Alisema Nivyema wanawake wawezekuchukua mikopo kwenye Benki kwa malengo Maalumu.

"Nawashauri wa Dada waweze kukopa sehemu sahihi na sehemu sahihi ni Benki na wakope kwa malengo Maalumu".Alisisitiza Venasia Msita.

0/Post a Comment/Comments