SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KUHAKIKISHA USALAMA WA MTOTO MTANDONI

.....................

Na Magrethy Katengu

Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu imesema inakwenda kuweka Mkakati Madhubuti  ikiwemo kufanya mapitio ya sheria na kanuni itakayokwenda kusaidia kudhibiti  Ukatili wa watoto Mtandaoni.

 Ameyasema hayo Jijini Dar es salaam Waziri Wa Maendeleo ya Jamii Jinsia wanawake  na Makundi  Maalumu Dkt Dorothy Gwajima wakati akifungua  Semina ya Usalama wa Mtoto Mitandaoni  kwa Wahariri na Waandishi wa vyombo vya habari ambapo   amesema  Wazazi ,   Teknolojia inakwenda kwa kasi na  na maudhui yanayosambaa mtandaoni ni hatari kwa watoto  hivyo Elimu haina budi kutolewa kwa  walezi kwani  wamejisahau na kuwapa watoto hao vifaa vya kielektroniki ikiwemo simu Tv pasipo kuwa  karibu nao kujua nini wanakitazama  watoto 

Waziri Dkt Gwajima amesema sambamba na hayo utaafiti uliyofanywa mwaka 2022 kwa watoto  Tanzania unaonyesha  umri wa miaka 12 hadi 17 ilibainika  asilimia 67 ya watoto wanaotumia mitandao maarufu ikiwa  ni pamoja na Facebook, Twitter (X), Instagram, Whatsap, Tiktok na Telegram na  asilimia 4 ya watoto waliotumia mitandao walifanyiwa aina tofauti za

ukatili kwenye mitandao  na wahalifu mtandaoni  waliwasiliana  huku asilimia 5 ya walishawishiwa au kulazimishwa kwa vitisho kutuma picha zao za utupu hivyo uangalifu unahitajika kwani licha faida nyingi za mitandaoni, athari zinazowakuta ni kutokana na kukosa uangalizi wa karibu.

Sanjari na hayo athari zinazotokea ambapo mlezi anakuwa hajui anashtuka mtoto kashaharibikiwa ikiwemo  kuanza ngono katika  umri mdogo hivyo kupata tatizo la  kisaikolojia na mmonyoko wa maadili  hii imechangia  kuwepo  vitendo vingi vya ukatili watoto kwa watoto kutokana na kuiga mtandaoni ikiwemo   mwingiliano wa mila na desturi za mataifa mengine  kuiga ushoga na usagaji.

"Tunakwenda  kutoa muarobaini      kuweka mikakati na   za kisera na kisheria za Kimataifa, Kikanda na Kitaifa katika kuwalinda watoto na Vijana wa Balehe dhidi ya ukatili wa Mitandaoni zikiwemo Sheria ya Makosa ya Kujamiiana Na. 4 ya 1998 kifungu cha 12, Aidha, Vifungu vya 12 na 13 vya Kanuni za Maudhui mitandaoni, 2018 chini ya Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta ya

2010, Kifungu cha 13 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao, ya 2015 na Vifungu

vya 83 na 158 (1) na (b) vya Sheria ya Mtoto Na.21, 2009" amesema Waziri 

   Wazazi na Walezi tatizo tutasaidia na vyombo vya habari  kutoa elimu ya uelewa kuhusu Ukatili wa Mtoto mtandaoni namna ya kujilinda pia tutafanya mapitio ya sheria na kanuni na kusogea kwenye teknolojia ili mtoto anapotumia vifaa vya teknolojia anakuwa salama hadhuriki na chochote ili tutengeneze kizazi kilicho bora na salama kinachotegemewa miaka ya usoni" amesema Waziri 

Sambamba na hayo amesisitiza kuwa lazima Maudhui yasiyofaa yasimfikie mtoto kwani Wazazi na Walezi lazima wawe kipaumbele kutimiza wajibu wa kuwa karibu na vifaa vya kiektroniki kwa watoto wao  wanavyovitumia kwa  kuwaawekea muda maalumu  kutumia vifaa kwani wengine hawalali wanakesha wakichati  usiku kucha.

Kwa upande wake Yusuphu Kileo Mtaalamu wa Masuala ya Mtandao na Uchunguzi wa makosa  ya kidigitali amesema Dunia ilivyo sasa mtoto mdogo wa miaka anaweza kuiwasha simu akatafuta kile anachokihitaji ikiwemo katuni hivyo baadhi ya nchi ilipogundua hilo zimeanza kuchukua hatua na Tanzania haijabaki nyuma mikakati inaanza mapema kwa kuanza na kuongezewa nguvu Sheria na taratibu kwani haizuiwi mtoto kutumia teknolojia lakini lazima Elimu itolewe kwanza   matumizi sahihi ya mitandao 

Sanjari na hayo amesema kumekuwa na tabia ya Wazazi kuwapa watoto simu pasipo kujua nini wanachokizatama mtandaoni hivyo amesema kabla ya Mtoto kupatiwa simu apatiwe elimu kwani wengine hutumia kutuma.picha na kuandika jumbe pasipo kujua kesho yake inaweza kuwaathiri hivyo sasa Wazazi walezi tambueni kuwa teknolojia ni nzuri lakini je wako anachokitazama kinaendana na yeye .

" Mzazi Mlezi hakikisha Usimwachie Mtoto wako kifaa cha kielektroniki kama hujui nini anachokitazama bora umnyang'anye kwani utakuwa unamsaidia sana atasoma vizuri hadi pale atakapopata kabla ya kumpatia simu mpatie elimu kwanza na kuwa karibu naye anachokitazama kwani kuna wengine walikurupuka na sasa wanajutia kuko

Aidha Februari 10 inatarajiwa kuafanyika tukio kubwa Dodoma la Uzinduzi wa kampeni usalama wa Mtoto Mtandaoni   na uzinduzi wa Kamati ya

Ushauri ya Taifa ya Usalama wa Watoto Mtandaoni itakakayoongoza  kampeni kauli mbiu ni “Usalama wa Mtoto Mtandaoni ni Jukumu letu Chukua hatua".

 

0/Post a Comment/Comments